Emir Sanusi alikuwa gavana wa benki kuu ya Nigeria kabla ya kuteuliwa kama Emir Kaskazini mwa Nigeria
Emir
wa Kaskazini mwa Nigeria, ambaye ni mmoja wa viongozi wa kiisilmau
wenye ushawishi mkubwa, ametoa wito kwa watu nchini humo kuchukua silaha
na kujilinda dhidi ya mashambulizi ya kundi la wanamgambo wa kiisilamu
wa Boko Haram.
Emir huyo wa Kano, Muhammad Sanusi, amewaambia wakazi wasisubiri wanajeshi kuwalinda kutokana na magaidi. Emir
huyo ambaye alikuwa gavana wa benki kuu nchini humo kabla ya kuchukua
wadhifa wake wa Emir, alitoa matamshi yake ya kutatanisha kwenye mkutano
wa maombi. Mwandishi wa BBC nchini Nigeria amesema kauli kama hii
sio kawaida kutolewa kwani Emir huyo huyo hazungumzii sana maswala ya
kisiasa.
Wapiganaji wa Boko Haram wamekuwa wakiwahangaisha wananchi kwa miaka mitano sasa
Wapiganaji wa wa Boko Haram
wanaendelea kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika sehemu kadhaa
za Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, huku wakiteka miji na mijiji ambko
wamekuwa wakiwataka wakazi kufuata sheria kali ya kiisilamu. Sanusi
alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali alipokuwa anafanya kazi yake ya
benki, alisema kuwa watu hawapaswi kuogopa wanamgambo hao na kwamba
wanapaswa kufanya wawezalo kujikinda kutokana na mashambulizi ya kundi
hilo. Mwandishi wa BBC anasema ingawa Emir huyo hakutaka kundi la
Boko Haram, ilikuwa hatua ya kipekee kwa kiongozi kama huyo kuwataka
watu kujihami dhidi ya Boko Haram. Aanasema hii ni dalili tu ya mambo yalivyo nchini humo hasa katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria
Wapiganaji wa Boko Haram wamekuwa wakiwahangaisha wananchi kwa miaka mitano sasa
wapiganaji wa wa Boko Haram wanaendelea kufanya mashambulizi ya mara
kwa mara katika sehemu kadhaa za Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, huku
wakiteka miji na mijiji ambko wamekuwa wakiwataka wakazi kufuata sheria
kali ya kiisilamu. Sanusi alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali
alipokuwa anafanya kazi yake ya benki, alisema kuwa watu hawapaswi
kuogopa wanamgambo hao na kwamba wanapaswa kufanya wawezalo kujikinda
kutokana na mashambulizi ya kundi hilo. Mwandishi wa BBC anasema
ingawa Emir huyo hakutaka kundi la Boko Haram, ilikuwa hatua ya kipekee
kwa kiongozi kama huyo kuwataka watu kujihami dhidi ya Boko Haram. Aanasema hii ni dalili tu ya mambo yalivyo nchini humo hasa katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Baada ya mashabiki wa mwanadada Wema "kumjia juu mwanamuziki Diamond Platnumz" kuhusu
tuhuma za yeye kumtumia mwanadada huyu kimwili zaidi bila kumuendeleza,
hatimaye raisi huyu wa kundi la WCB ameamua nay eye kufunguka haya
mazito juu ya kauli hizo. Kupitia ukurasa wake wa mtandao ule maarufu wa
kijamii Diamond ameandika haya..
“Nafkiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya
dhati kwa Msanii wenu... kama mngemshauri apunguze Mashoga wapenda anasa
na apunguze Stareh zisizo na Faida, wenda ingemsaidia Pesa kuzitumia
kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya
pombe... Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha Mpenzi
wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumuwezesha
mtaji wa kufanyia kazi. Waswahili wanasema Mchungaji bora anatakiwa
kuhakikisha anampeleka Ng'ombe wake Kwenye Maji safi....ila yeye ng'ombe
mwenyewe ndio anatakiwa aamue kunywa maji!!!!! Au mnataka nikishampa
mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie ????
Nisiende Studio nikae dukani nimuuzie mie????.. ni juhudi zako
kwanza!... leo hii mimi Hata ningepewa Mamilioni ya mamilioni kama
nisingekuwa na moyo wa mie mwenyewe kwanza kutaka kujituma na kupenda
kufanya kazi yangu nisingefikia hapa nilipo!....Mxieeeeeeeew!
Polisi nchini Kenya wamefanya msako
mkali dhidi ya misikiti inayotoa mafunzo ya itikadi kali za kidini mjini
Mombasa pwani ya Kenya.
Mtu mmoja ameuawa kwenye msako huo
ulioanzishwa Jumapili dhidi ya misikiti inayosemekana kutoa mafunzo ya
kuunga mkono harakati za kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab
nchini Somalia.
Misikiti ya kwanza kulengwa katika msako huo ni ile ya Masjid Musa na Sakina.
Mkuu
wa polisi mjini Mombasa alinukuliwa na shirika la habari la AFP akisema
kuwa walipata taarifa kwamba kundi hilo limekuwa likipanga kufanya
mashambulizi na hiyo ndiyo sababu ya msako huo kuanzishwa.
Mabingwa watetezi wa kombe la Afrika
Nigeria wameicharaza Congo Brazaville 2-0 siku ya jumamosi ili
kuimarisha matumaini yake ya kufuzu katika dimba la Afrika mwaka 2015
huku Afrika kusini na Cameroon zikifuzu katika kinya'nganyiro hicho.
Afrika
kusini iliichapa Sudan 2-1 katika mechi yao ya kwanza tangu kuuawa kwa
mlinda lango wake Senzo Meyiwa ili kuongoza kundi la Da. Zambia nayo iliinyamazisha Mozambique 1-0 mjini Moputo kufuzu na katika kundi Fa pamoja na viongozi wa kundi hilo Cape Verde. Burkina
Faso na Gabon pia zilifuzu katika kundi Cha baada ya Kuishinda Lesotho
1-0 mjini Maseru huku Angola ikipata sare ya bila kwa bila dhidi ya
wenyeji wake mjini Luanda.
Shughuli za bunge zimekwama kutokana na tofauti zilizopo kati ya waziri kuu na rais wa SomaliaHassan Sheik Mohamud. Wadadisi wanasema kuwa hali imedhoofika kutokana na mizozo ya kisiasa. Marekani inasema kuwakura hiyo ya kutokuwa na imani haiwakilishi maslahi ya raia.
Wanasanyansi wa safari za anga za mbali wamejawa na shauku ya kutaka thibitisho kwamba Chombo kilichopelekwa na kutua kwenye kimondo au nyota mkia yaani Comet iliyo umbali wa zaidi ya kilometa nusu bilioni kutoka duniani.
Hapo jana Chombo hicho kiliwezesha kuwekwa kwa historiaya kuwa kifaa cha kwanza kuwahi kutengenezwa na binadamu kutua kwenye kimondo, kazi iliyochukua zaidi ya miaka 10. Hata hivyo huenda bado kifaa hicho hakijajibanza kwenye kimondo hicho chenye upana wa kilometa mbili , kama ilivyotarajiwa-Data mpya na hasa picha zinasubiriwa kwa hamu kubwa.
Mbinu mpya mbalimbali zinahitajika kwa ajili ya kupambana na virusi vya Ebola nchini Liberia, shirika la madaktari wasio na mipaka, MSF limeeleza.
Zaidi
ya Watu 6,000 wameathiriwa na ugonjwa huo nchini Liberia lakini takwimu
zinaonyesha kuwa idadi ya maambulizi mapya imeendelea kupungua.
MSF imesema kuwa imekuwa na uwezo mkubwa wa kuwa na vituo vingi vya kupambana na maradhi hayo kuliko idadi ya wagonjwa. Mfano kituo kimoja mjini Monrovia
kilikua na vitanda 250 lakini kimekua kikitibu wagonjwa 50 pekee, hivyo
shirika hilo limeomba kubadilishwa kwa mbinu za mapambano dhidi ya
ebola Liberia ni nchi iliyoathirika zaidi na ugonjwa wa
Ebola kwa karibu ya nusu ya idadi ya walioathiriwa wa ugonjwa huo Afrika magharibi. Hivi sasa kiasi cha maambukizi kinaendelea kuwa juu nchini Guinea na Sierra Leone