VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Saturday, May 14, 2016

Mamia mkoani Mbeya wajitokeza kumzika Kinyambe


        Mamia ya watu wamejitokeza Ijumaa hii mkoani Mbeya 
  kwa ajili ya mazishi ya mchekeshaji maarufu nchini Tanzania kutoka katika Kundi la Vituko Show, Mohammed Abdallah ‘Kinyambe’ aliyefariki dunia Jumatano iliyopita akiwa katika hospitali ya Mbeya.
????????????????????????????????????
Mmoja kati ya wasanii wanaounda Chama Cha Wasanii Wachekeshaji Tanzania, Mkono Mkonole, kupitia ukurasa wake wa instagram ameandika:
Kila nafsi itaonja umahuti kwa heri kinyambe kila mwanadamu huu ndio mwisho wake pumzika kwa amani
Mkonole aliiambia Bongo5 Alhamisi hii, kuwa Kinyambe alikuwa anasumbuliwa na uvimbe tumboni mpaka anapatwa na umahuti akiwa nyumbani kwao Mbeya.
Mazishi yake yamehudhuriwa na wananchi, wadau wa filamu pamoja na wasanii wenzake wa filamu ambao walisafikiri kutoka Dar es salaam.


VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

Monday, May 2, 2016

Prof. Lipumba Apongeza Mipango ya Rais Magufuli



Mwanasiasa mkongwe ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya uchumi nchini Profesa Ibrahimu Lipumba amesema anaunga mkono mpango wa serikali wa miaka mitano huku akisema ni vema serikali ihakikishe inawekeza zaidi katika nishati ya umeme ili kufikia lengo la kuwa nchi ya viwanda.

Wakati tayari mpango wa serikali ukiwa umekwishawasilishwa kwa miaka mitano ijayo, ambapo umeanisha namna utakavyofanikisha asilimia 40 ya ajira ifikapo mwaka 2020 zikitokana na viwanda, huku miongoni mwa miradi mikubwa uinayotarajiwa kutekelezwa ya viwanda ni ujenzi wa kiwanda cha chuma.

Aidha Mchumi huyo pia amesema adhima ya serikali ya kujenga nchi ya viwanda itafanikia ikiwa itawekeza katika nishati ya umeme wa uhakika, licha ya miradi mikubwa kama ya Power Afrika na MCC kusitishwa huku akiishauri serikali kufanyia kazi maazimio ya bunge kuhusu sakata la Tegeta esrow.

Mahojiano hayo maalum yamefanyika Dar es Salaam, muda mfupi baada ya Prof Lipumba kupokea ujumbe maalum wa wawafuasi wa chama cha CUF kutoka mjini bagamoyo waliokuwa lengo la msihi kurejea kwenye nafasi yake ya uenyekiti wa chama cha CUF.

VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

Tuesday, April 19, 2016

Video 8 za Mambo Yote Yaliyojiri Bungeni Dodoma Leo





1.Hatimaye mkutano wa kwanza kikao cha 3 wa bunge waanza kwa wabunge kuimba wimbo wa taifa na baadhi yao kula kiapo.
 https://www.youtube.com/watch?v=iV2ZYeyJyRU#action=share
 
2.Je ni nini hatma ya uchaguzi kwa majimbo ya Bulyankulu na kamindo ikiwa uchaguzi haujafanyika hadi leo? Dkt. Abdallah Possy atoa ufafanuzi. 
 
3.Mhe. Suleiman Jafo atoa ufafanuzi na utaratibu wa serikali juu ya hospitali zinazopandishwa hadhi kukidhi haja za wananchi.
 
4.Mbunge wa Njombe mjini aihoji serikali juu ya upigaji marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki unaosababisha uharibifu wa mazingira. 
 
5.Naibu waziri wa nishati na madini Dkt Medard kalemani atoa ufafanuzi wa kuanza kwa mradi wa kuzalisha umeme wa Malagarasi. 
 
6.Je serikali inaweka msukumo gani kwa Geita Gold Mining kuhakikisha inawalipa wananchi wa mtaa wa Mgusu fidia ili kupisha eneo hilo? 
 
7.Kauli ya Wizara ya mambo ya ndani kuhusu baadhi ya vituo vya polisi nchini kuwa na askari wachache na kutofanya kazi kwa masaa 24.
 
8.Je ni lini uwanja wa ndege wa Musoma utajengwa na kuwa kwenye hadhi ya stahiki ya kitaifa au kimataifa? Mhe. Joyce Sokombi ahoji.

VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

Friday, April 15, 2016

Bibi Kizee Abakwa Mkoani Singida



Pichani ni Bibi kizee mwenye umri wa miaka 84 na mkazi wa Kijiji cha Chungu, tarafa ya Ihanja, wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida akiwa amebebwa na mmoja wa ndugu zake wakati akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya mjini Singida kutoa ushahidi katika kesi inayomkabili kijana mmoja mwenye umri wa miaka 32 (jina lake halikupatikana) anayetuhumiwa kumbaka bibi kizee huyo kwa mara ya tatu sasa ndipo walipofanikiwa kumkamata. (Picha Na Jumbe Ismailly)
VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

Monday, April 11, 2016

KITUMBUA Kimeingia Mchanga...Ikulu Yafuta Safari ya Wakuu wa Wilaya 10 Kwenda China China




Katibu Mkuu Kiongozi John Kijazi

Ikulu imefuta safari ya wakuu wa wilaya 10 na wakurugenzi idadi kama hiyo waliotakiwa kwenda China kwa mafunzo ya uchumi wa kimaeneo kuanzia jana, na kuna uwezekano mkubwa ikatangaza uteuzi mpya leo.

Wakuu hao wa wilaya na wakurugenzi wao  walikuwa waondoke jana kwa ufadhili wa Serikali ya Watu wa China, lakini habari zinaarifu kuwa Ikulu iliamua kutotoa kibali, hali inayozidisha ubashiri kuwa uamuzi huo umetokana na kukamilika kwa uteuzi wa wakuu wapya.

Safari hiyo ilishakamilika kwa kiwango kikubwa baada ya kupata visa na wengi wao kuwasili jijini Dar es Salaam tayari kwa safari hiyo, lakini wakalazimika kurejea kwenye vituo vyao baada ya kukosa kibali cha Ikulu ambacho hutolewa na Katibu Mkuu Kiongozi.

Mara tu baada ya kuapishwa Novemba 5 mwaka jana, Rais John Magufuli alitangaza kudhibiti safari za nje za watumishi na viongozi wa umma kwa kuagiza kuwa Ikulu ndiyo itakayotoa kibali baada ya kujiridhisha na umuhimu wa safari hizo kwa Taifa.

Tangu atoe agizo hilo, ni mawaziri wawili tu ambao wameruhusiwa kwenda Vietnam kwenda kujifunza kilimo na viwanda. Mawaziri hao ni Mwigulu Nchemba (Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi) na Charles Mwijage (Viwanda na Biashara).

Naibu Waziri wa Fedha, Dk Ashatu Kijaji alikwenda nchini Ethiopia kuhudhuria mkutano wa mawaziri wa fedha, wakati kwa nyakati tofauti Makamu wa Rais Samia Suluhu na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa walikwenda Afrika Kusini na Botswana.

Mpaka sasa, Rais Magufuli amefanya safari moja tu ya nje alipokwenda Rwanda kwenye maadhimisho ya mauaji ya kimbari.

Lakini safari ya wakuu hao wa wilaya ilikuwa ifadhiliwe na China, kwa mujibu wa habari hizo na hivyo isingeisababishia Serikali kutumia vibaya fedha za walipa kodi.

Uamuzi huo unaonekana kuzingatia zaidi uteuzi wa wakuu wapya ambao taarifa zinasema unaweza kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa, wakati wa wakurugenzi wa wilaya unatazamiwa kutangazwa baadaye wiki hii au wiki ijayo.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene alikiri kuwapo kwa safari hiyo, lakini akasema hajui kama imeidhinishwa na Ikulu kwa kuwa si muhusika.

“Katika hatua za awali nilisaini safari hiyo kuwaruhusu waende China, lakini sijui kama wamenyimwa kibali kwa sababu hilo si suala la ofisi yangu,” alisema Waziri Simbachawene.

Kama ni kweli, alifafanua Simbachawene, inaweza kuwa ni kutokana na umuhimu wao wa kuwatumikia wananchi kwenye maeneo wanayotoka. “Hawawezi kuondoka na kuziacha wilaya zao ilhali wao ndiyo waangalizi,” alisema Simbachawene.

Akiwa Chato mkoani Geita, Rais aliwataka wakuu wa wilaya kuchapa kazi badala ya kuwa na woga wa kutoteuliwa akisema uchapaji kazi ndio utawafanya waendelee kuwapo kwenye nafasi zao.

Rais pia amekuwa akitoa maelezo kadhaa yanayoonyesha atafanya uteuzi kwa kutumia vigezo hivyo, hasa suala la elimu ambayo inakabiwa na tatizo kubwa la uhaba wa madawati na vyumba na majengo, kipindupindu, njaa, migogoro ya ardhi na watumishi hewa.






VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

Monday, March 28, 2016

Dk Shein amteua Balozi Seif Ali Idd Kuwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar



Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein amemteua Balozi Seif Ali Idd kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa visiwa hivyo.

Kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 39 (2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Dk Shein amemteua Balozi Idd ambaye alikuwa na wadhifa huo hata kipindi kilichopita.

Uteuzi wa Balozi Idd aliyezaliwa Februari 23, mwaka 1942, ulianza jana ikiwa ni siku nne tangu kuapishwa kwa Shein kuwa Rais wa Zanzibar.

Balozi Idd anakuwa mtu wa pili kuteuliwa na Dk Shein baada ya kuteuliwa kwa mwanasheria mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said mwishoni mwa wiki.

Dk Shein sasa atakuwa na wakati mgumu wa ama kumteua au kutomteua Makamu wa Kwanza wa Rais ili kukidhi matakwa ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) kwani hakuna chama cha upinzani kilichokidhi vigezo vya kushirikishwa katika kuunda Serikali.

VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......