Tuesday, May 23, 2017
Sunday, January 29, 2017
BREAKING: Picha 13 za uokoaji kwa waliofukiwa mgodini Geita













VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......
Monday, December 26, 2016
RATIBA KAMILI YA MAPINDUZI CUP
KUNDI A: Simba, URA, KVZ, Taifa ya Jangombe na Jangombe Boys.
KUNDI B: Yanga, Azam, Zimamoto na Jamhuri.
RATIBA KAMILI YA MAPINDUZI CUP
30/12/2016 Taifa ya Jang’ombe vs Jang’ombe boys saa 2:30 usiku.
1/1/2017 KVZ VS URA Saa 10:00 alasiri, Simba vs Taifa ya Jang’ombe saa 2:30 usiku.
2/1/2017 Azam vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Jamhuri saa 2:30 usiku.
3/1/2017 Jang’ombe boys vs URA saa 10:00 alasiri, KVZ vs Simba saa 2:30 usiku.
4/1/2017 Zimamoto vs Yanga saa 10:00 alasiri, Jamhuri vs Azam saa 2:30 usiku.
5/1/2017 KVZ vs Jang’ombe boys saa 10:00 alasiri, Simba vs URA saa 2:30 usiku.
6/1/2017 Taifa ya Jang’ombe vs KVZ saa 2:30 usiku.
7/1/2017 Jamhuri vs Zimamoto saa 10:00 alasiri, Yanga vs Azam saa 2:30 usiku.
8/1/2017 Simba vs Jang’ombe boys saa 10:00 alasiri ,Taifa ya jang’ombe vs URA 2:30 usiku.
10/1/2017 Saa 10: 00 nusu fainali ya kwanza , Saa 2:30 nusu fainali ya pili.
13/1/2017 Fainali saa 2: 30 usiku.
VITUS MTAFYA
..... ILEJE NI NYUMBANI ......Wednesday, December 14, 2016
BREAKING NEWS : KUTOKA MWANJELWA
madereva bajaji wafunga barabara baada ya wenzao 42 kufikishwa mahakamani
Baada ya madereva 42 kufikishwa mahakamani
vurugu kubwa zimezuka eneo la Block T jijini Mbeya baada ya vijana kufunga barabara hiyo kwa mawe na kuleta adha kubwa kwa watumiaji wa barabara.
VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......
Monday, December 5, 2016
Mwanafunzi wa darasa la 5 Ajinyonga
Mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kizota mjini Dodoma, Yasin Abdallah (13) amekutwa amejinyonga bafuni nyumbani kwao baada ya kuchukizwa kufanya vibaya kwenye masomo yake.
Kaimu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Ernest Kimoli alisema tukio hilo
lilitokea Desemba 2 eneo la Kizota Relini Manispaa ya Dodoma.
Kimoli alisema baba mzazi wa mtoto huyo, Hassan Juma (53) aligundua kujinyonga kwa mwanaye saa 6:00 mchana.
“Sababu ya kujinyonga ni kuchukizwa na matokeo ya mitihani yake,” alisema.
Diwani wa Kizota, Jamary Ngalya alisema mtoto huyo ambaye alizikwa juzi jioni, alianza kwa kuwaeleza wanafunzi wenzake Ijumaa kuwa atajinyonga.
Diwani wa Kizota, Jamary Ngalya alisema mtoto huyo ambaye alizikwa juzi jioni, alianza kwa kuwaeleza wanafunzi wenzake Ijumaa kuwa atajinyonga.
Alisema
baada ya kutamka maneno hayo, wenzake walimwambia wanakwenda kumweleza
mwalimu. Hata hivyo, baada ya kuwasikia wenzake aliwaambia kuwa anatania
hawezi kufanya hivyo.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Kizota, Juma Malecela alisema mwanafunzi huyo alihamia Oktoba kutoka mkoani Kigoma.
“Katika matokeo ya kumaliza darasa la nne alikuwa wa 129 kati ya 132, inawezekana huko alikuwa anafanya vizuri,” alisema.
VITUS MTAFYA
..... ILEJE NI NYUMBANI ......“Katika matokeo ya kumaliza darasa la nne alikuwa wa 129 kati ya 132, inawezekana huko alikuwa anafanya vizuri,” alisema.
Friday, November 25, 2016
Mchungaji Anthony Lusekelo (Mzee wa Upako) akamatwa na Polisi.....Anadaiwa Kumfanyia Fujo Jirani Yake
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Dar es Salaam, Anthony Lusekelo, maarufu Mzee wa Upako, amekamatwa na polisi akituhumiwa kumfanyia fujo na kutishia kumuua jirani yake.
Tukio
hilo lilitokea juzi maeneo ya Kawe wilayani Kinondoni, Dar es Salaam,
kuanzia saa 11 asubuhi hadi saa tatu alipochukuliwa na polisi wa Kituo
cha Kawe.
Wakati
wa tukio hilo, Mchungaji Lusekelo alikuwa ameegesha gari lake
barabarani kiasi cha kusababisha usumbufu na foleni ya magari mengine.
Chanzo
cha tukio hilo kinadaiwa ni kulipiza kisasi kwa jirani zake hao
wanaoishi katika nyumba namba KAW/MZN/1348, ambao alidai wamekuwa
wakimkebehi kuwa hafai kuwa mchungaji kwa sababu ya ulevi.
Licha
ya baadhi ya watu kumsihi aondoke eneo hilo kutokana na hadhi yake,
mchungaji huyo alikaidi, huku akiendelea kuongea kwa sauti iliyofanana
na mtu mwenye kilevi.
Baadhi ya maneno yaliyosikika kwenye video iliyorekodiwa eneo la tukio hayaandikiki kwa kuwa si ya kawaida.
“Mjinga wewe, mimi ni zaidi ya askari na wewe ni mgambo, na si mgambo wewe ni raia tu.
“Umenitukana
sana wewe mpaka leo nimeamua kuloana na mvua, usitoe gari hapo mshenzi
sana wewe, na nikikuona mahali popote…, mshenzi kabisa, muangalie sana
huyo,” alisikika Mchungaji Lusekelo akiongea kwa sauti.
Baada ya kuongea maneno hayo, ilisikika sauti ya mwanamke kutoka ndani ya uzio wa nyumba hiyo ikimjibu mchungaji huyo: “Huwezi, aniangalie kitu gani.”
Hata
hivyo, hata watu mbalimbali walipomsihi aache kutoa lugha hizo za
kejeli na aondoe gari lake lililokuwa limesababisha foleni, alikataa
akisema hataliondoa hadi atakapokuja Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya
Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro.
Baada
ya purukushani hizo, polisi kutoka katika Kituo cha Kawe walifika eneo
hilo saa tatu asubuhi, wakamchukua mchungaji huyo na kumpeleka kituoni.
Inadaiwa
baada ya kufikishwa kituoni hapo, mchungaji huyo alipimwa kiwango cha
ulevi na kukutwa 131, ambacho kinaelezwa kuwa ni kikubwa – ulevi wa
kupindukia.
Ilipofika
saa tano asubuhi, mchungaji huyo alihamishiwa Kituo Kikuu cha Polisi
(Central), ambako huko nako inadaiwa alipimwa kilevi na kuonekana
kushuka hadi kufikia 121.
Alipotafutwa
Kamishna Sirro ili kuzungumzia sakata la mchungaji huyo, alisema
atalizungumzia leo katika mkutano wake na waandishi wa habari.
VITUS MTAFYA
..... ILEJE NI NYUMBANI ......Tuesday, August 23, 2016
Lowassa Apigilia Msumari Oparesheni UKUTA, Asema Haiwezekani Mtu Mmoja Azuie Kila Kitu
UKUTA si fujo , UKUTA si machafuko na hatuna haja ya kufanya fujo , tunapiga kelele dhidi ya uvunjwaji wa haki ya kidemokrasia na katiba ya nchi unaofanywa na utawala huu wa awamu ya tano .
CHADEMA ni nani wakapambane na polisi ,polisi ambao ni watoto wetu ,ndugu zetu na hata wake na waume zetu ila tuwahakikishie hatutorudi nyuma pale katiba na haki ya kidemokrasia ikichezewa au kuwa chini ya mtu fulani .
Najua polisi watapiga watu ,wataumiza watu na hata kuua ila niwahakikishie wao na walio na mamlaka wataishia katika mahakama ya Kimataifa .
Siasa ni mazungumzo ,lazima tuzungumze milango yetu iko wazi kufanya mazungumzo ila kwa kuwa hawahitaji na sisi hatutorudi nyuma September Mosi ,tumejiandaa vya kutosha na sasa tuko ngazi ya kaya na wajumbe wetu wanakamilisha kazi katika kaya ili tarehe mosi sauti ya kutosha ipazwe kwa maandamano na mikutano kama tulivyokubaliana katika kata zetu na majimbo nchi nzima .
Haiwezekani hata kidogo mtu mmoja azuie kila kitu ,nchi hii ni mali yetu sote na inaongozwa na Katiba na sheria.
Kamati kuu ilipoamua katika suala la UKUTA haikukurupuka , kamati kuu yetu inaundwa na mchanganyiko wa wasomi wa kada mbalimbali ,wazee wenye busara na vijana machachari kamwe hawawezi kukukurupuka na UKUTA ni haki ya watanzania wote.
Pili naomba niwape siri ya ushindi 2020 ndugu zangu na wanachama wenzangu , tutashinda uchaguzi Mkuu 2020 kama tutafanya yafuatayo na kuyasimamia
Kwanza; Umoja ndani ya Chama na wanachama ,tuheshimiane ,tusameheane na tuimarishe chama chetu
"chama ndani ya Chama , chama nje ya chama na chama ndani ya Umma "- LOWASSA
VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......
Subscribe to:
Posts (Atom)





