VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Tuesday, February 2, 2016

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JKT



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama , Dk John Pombe Magufuli amemteua Brigedia Jenerali MW Isamuhyo kuwa mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamnyange amesema uteuzi wa Brigedia Jenerali Isamuhyo kuwa Mkuu wa JKT unafuatia kustaafu utumishi jeshini kwa Meja Jenerali Raphael Muhuga baada ya kufikisha umri wa kustaafu kisheria.
Meja Jenerali Muhuga amestaafu utumishi Jeshini tarehe 31 Januari 2016 baada ya kutumikia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa muda wa miaka 43, ikiwemo miaka mitatu akiwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).

IMETOLEWA NA

KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO,

MAKAO MAKUU YA JESHI LA KUJENGA TAIFA,

LEO TAREHE 30 JANUARI 2016


VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

No comments: