VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Saturday, May 14, 2016

Mamia mkoani Mbeya wajitokeza kumzika Kinyambe


        Mamia ya watu wamejitokeza Ijumaa hii mkoani Mbeya 
  kwa ajili ya mazishi ya mchekeshaji maarufu nchini Tanzania kutoka katika Kundi la Vituko Show, Mohammed Abdallah ‘Kinyambe’ aliyefariki dunia Jumatano iliyopita akiwa katika hospitali ya Mbeya.
????????????????????????????????????
Mmoja kati ya wasanii wanaounda Chama Cha Wasanii Wachekeshaji Tanzania, Mkono Mkonole, kupitia ukurasa wake wa instagram ameandika:
Kila nafsi itaonja umahuti kwa heri kinyambe kila mwanadamu huu ndio mwisho wake pumzika kwa amani
Mkonole aliiambia Bongo5 Alhamisi hii, kuwa Kinyambe alikuwa anasumbuliwa na uvimbe tumboni mpaka anapatwa na umahuti akiwa nyumbani kwao Mbeya.
Mazishi yake yamehudhuriwa na wananchi, wadau wa filamu pamoja na wasanii wenzake wa filamu ambao walisafikiri kutoka Dar es salaam.


VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

Monday, May 2, 2016

Prof. Lipumba Apongeza Mipango ya Rais Magufuli



Mwanasiasa mkongwe ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya uchumi nchini Profesa Ibrahimu Lipumba amesema anaunga mkono mpango wa serikali wa miaka mitano huku akisema ni vema serikali ihakikishe inawekeza zaidi katika nishati ya umeme ili kufikia lengo la kuwa nchi ya viwanda.

Wakati tayari mpango wa serikali ukiwa umekwishawasilishwa kwa miaka mitano ijayo, ambapo umeanisha namna utakavyofanikisha asilimia 40 ya ajira ifikapo mwaka 2020 zikitokana na viwanda, huku miongoni mwa miradi mikubwa uinayotarajiwa kutekelezwa ya viwanda ni ujenzi wa kiwanda cha chuma.

Aidha Mchumi huyo pia amesema adhima ya serikali ya kujenga nchi ya viwanda itafanikia ikiwa itawekeza katika nishati ya umeme wa uhakika, licha ya miradi mikubwa kama ya Power Afrika na MCC kusitishwa huku akiishauri serikali kufanyia kazi maazimio ya bunge kuhusu sakata la Tegeta esrow.

Mahojiano hayo maalum yamefanyika Dar es Salaam, muda mfupi baada ya Prof Lipumba kupokea ujumbe maalum wa wawafuasi wa chama cha CUF kutoka mjini bagamoyo waliokuwa lengo la msihi kurejea kwenye nafasi yake ya uenyekiti wa chama cha CUF.

VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......