VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Friday, February 27, 2015

HOSPITAL YA MISSION YA IGOGWE TUKUYU WILAYANI RUNGWE YAWATELEKEZA WAGOJWA KUMI NA NNE WA AJALI YA MOTO SIKU NNE BILA YA MATIBABU NA KUPELEKEA MMOJA WAO KUFARIKI DUNIA.

WANANCHI WACHANGISHANA PESA NA KUWAHAMISHA WOTE NA KUANZA MATIBABU HOSPITAL YA WILAYA YA TUKUYU MAKANDANA

HAPA NDIPO HOSPITAL YA MISSION IGONGWE AMBAPO WAGONJWA WAPATAO KUMI NA NNE WALIFIKISHWA KWAAJILI YA KUPATA MATIBABU LAKINI WANANCHI WA KIJIJI CHA ISONGOLE KWA PAMOJA WALIPOONA NDUGU ZAO WAMETELEKEZWA KWA KUTOPATA MATIBABU YA KURIDHISHA NA KUPEREKEA KIFO CHA MGONJWA MMOJA NA KUFIKIA WATU WANNE WALIOKUFA KATIKA AJALI,  NDIPO WANANCHI WAMEAMUA KUCHANGISHANA PESA NA KUWAHAMISHA WAGONJWA WOTE NA KUWAPELEKA KATIKA HOSPITAL YA WILAYA YA RUNGWE AMBAPO WAGONJWA WOTE WAMEANZA MATIBABU

MMOJA WA WAGONJWA WALIOTELEKEZWA KUTOPATA HUDUMA KATIKA HOSPITAL YA IGOGWE. KINGOTANZANIA ILIPOFIKA KATIKA HOSPITAL YA TUKUYU WILAYANI RUNGWE IMESHUHUDIA HARI MBAYA ZA WAGONJWA KUMI NA TATU WALIOHAMISHWA NA WANANANCHI KUTOKA HOSPITAL YA IGOGWE KWA KUWA WAGONJWA HAO TANGU WALIPOFIKISHWA HOSPITAL WAMEKOSA HUDUMA ZA MSINGI INGAWA NDUGU WA WAGONJWA WOTE WALICHANGISHWA PESA KWA AJILI YA KUNUNUA DAWA LAKIN WAGONJWA WAMELALAMIKA KUKOSA HUDUMA ILIYOPELEKEA MWENZAO MMOJA KUFARIKI NDUNIA AKIWA HOSPITALIN HAPO

MMOJA WA MAJERUHI WA MOTO AKIWA KATIKA HOSPITAL YA IGOGWE KABLA YA KUHAMOSHIWA KWENDA KATIKA HOSPITAL YA WILAYA YA RUNGWE

HAPA NDIPO AJALI YA MOTO ILIPOTOKE KATIKA KIJIJI CHA ISONGOLE WILAYANI RUNGWE AMBAPO WATU WALIFARIKI DUNIA HAPOHAPO HUKU MAJERUHI WA NNE AKIFIA HOSPITALINI IGOGWE KWA KUKOSA HUDUMA ZA MSINGI

WANANCHI WA KIJIJI CHA ISONGOLE KWA PAMOJA WAKIONGOZWA NA MWENYEKITI NA DIWANI WAO WALIPOONA NDUGU ZAO WAMETELEKEZWA KWA KUTOPATA MATIBABU YA KURIDHISHA NA KUPEREKEA KIFO CHA MGONJWA MMOJA NDIPO WANANCHI WAMEAMUA KUCHANGISHANA PESA NA KUWAHAMISHA WAGONJWA WOTE NA KUWAPELEKA KATIKA HOSPITAL YA WILAYA YA RUNGWE AMBAPO WAGONJWA WOTE WAMEANZA MATIBABU

Thursday, February 26, 2015

Matukio mbalimbali ya ziara ya Waziri Mkuu Pinda Mbeya mjini na vijijini

PG4A2882
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wananchi baada ya kufungua vyumba vitatu vya Maabara katika shule ya sekondari ya Songwe mkoani Mbeya Febrari 25, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
PG4A2919
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwasikiliza wanafunzi wa shule ya sekondari ya Iwambe wilayani Mbeya wakati alipofungua na kukagua maabara tatu za shule hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Februari 25, 2015. Wapili kushoto ni mkewe Tunu na Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Norman Sigalla.
PG4A2988
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua soko Kuu la Mjini Mbeya la Mwanjelwa baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wake akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya, Februari 25, 2015.
PG4A3031
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wananchi wa Kijiji cha Kimondo, Mbeya Vijijini  kabla ya kuweka jiwe la Msingi la zahanati yao akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Februari 25, 2015. Kushoto kwake ni Mbunge wa Mbeya Vijijini, Luckson Mwanjale na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mbeya mjini Dr. Norman Sigalla.
PG4A3034
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka jiwe la Msingi la zahanati ya Kimondo , Mbeya Vijijini akiwa katika ziara ya mkoa  wa Mbeya, Februari 25, 2015. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini Dr. Norman Sigalla.
PG4A3046
Waziri Mkuu, Mizengo PInda akizungumza na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi la Zahanati  ya Kimondo, Mbeya Vijijini  akiwa katika ziara ya mkoa wa huo, Februari 25, 2015.
PG4A3074
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi la Zahanati ya Kimondo na kuzungumza akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya, Februari 25, 2015.
PG4A3106
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akihutubia Mkutano wa hadhara katika kijiji cha Igoma , Mbeya Vijijini akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mbeya Februari 25, 2015.
PG4A3137
Wasanii, Max Oswald (kushoto) na  Ivan Kina wakitumbuiza katika mkutano wa hadhara  uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika kijiji cha Igoma, Mbeya Vijijini Februari 25, 2015.

Breaking News: Chid Benz Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Miwili Jela au Kulipa Faini ya sh. 900,000


Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Rashidi Abdallah Makwaro Maarufu kama (Chid Benzi) amehukumiwa kifungo cha miaka mwili jela au kulipa faini ya shingili laki tisa bada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu ikiwemo kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin yenye thamani ya sh. 38,638, bangi ya sh. 1,720 na vifaa ya kuvutia dawa hizo kijiko na kigae.

Chid Benz alikamatwa mwaka jana katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akiwa na madawa hayo.
 
Mwanamuziki huyo ambaye alikiri kosa hilo wiki iliyopita, alikamatwa uwanjani hapo akiwa anajitayarisha kupanda ndege kwenda Mbeya kwenye tamasha la muziki.

Hata  hivyo, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo   imemwachia  huru mwanamuziki huyo  baada ya kulipa faini ya 900,000/

Monday, February 23, 2015

NACTE YAFUNGUA APPLICATION ZA AFYA CERTIFICATE,DIPLOMA NA DIGRII-SOMA HAPA (vitusmtafya.blogspot.com)


                                  
Baraza la mitihani nacte limefungua Usajili kwa wanafunzi wanaotaka kusomea afya cheti hadi digrii ambapo kwa mara ya kwanza chuo cha st.josephy chatoa digrii mpya ya clinical medicine miaka minne.

PUBLIC NOTICE - OPENING OF CAS
OPENING OF THE CENTRAL ADMISSION SYSTEM (CAS) FOR NEW APPLICANTS
MARCH INTAKE

The National Council for Technical Education (NACTE) would like to inform the public that Central Admission System (CAS) is now open for new applicants into:
1. Health Training Institutions (Ordinary Diploma and Certificate in Nursing) for  March 2015 intake into  the following institutions,
  • A3 Institute of Professional Studies - Ilala, DSM,
  • Mikocheni Nursing School - Dar es Salaam 
  • Massana College of Nursing - Dar-es-Salaam
  • St. Glory Nursing School- Dar-es-Salaam
  • Ilembula Institute for Health and Allied Science
  • Mbalizi Health Institute
  • Yohana Wavenza Health Institute
  • St. John College of Health Science
  • Isimila Nursing School
  • St. Aggrey College of Health Science
  • Tumaini University Makumiza – Mbeya Campus 
NOTE: All applications should be done online through www.nacte.go.tz and the deadline on this application will be on 13th March 2015.

2. Bachelor of Clinical Medicine for  March 2015 intake at St.Joseph University College of Health and Allied Sciences.
  • Duration: Four (4) years
  • Entry Requirement: Ordinary Diploma in Clinical Medicine (GPA 2.7 or above)
  • School fees: 6,260,400/=
  • Date of Commencement of Program: 20th April, 2015

Taarifa Rasmi ya Jeshi la Polisi Kuhusiana na Sakata la Kutekwa kwa Wanajeshi wa JKT Waliotaka kuandamana Kudai Ajira



Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia vijana watano wa kundi la wahitimu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa tuhuma za kufanya uchochezi na kufanya mikusanyiko isiyo halali jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema vijana hao wamekamatwa kwa nyakati tofauti kwa makosa ya kuunda kikundi kisicho halali kwa mujibu wa sheria za nchi na kuwahamasisha wenzao, kuandamana hadi Ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete kudai ajira za kudumu.
 
“Tunawashikilia vijana watano ambao ndio viongozi wa kikundi kinachojiita umoja wa wahitimu wa Jeshi la Kujenga Taifa. Mwenyekiti ndio alikuwa wa kwanza kukamatwa na wengine tuliwakamata juzi mara baada ya kukusanyika eneo la Msimbazi Centre na Muhimbili,” alisema Kova.
 
Akieleza chanzo cha vijana hao kutaka kuandamana kuelekea Ikulu, alidai wahitimu hao wanadai kuahidiwa ajira za kudumu walipomaliza mafunzo yao na hivyo baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kuajiriwa, ndipo wakaamua kuanzisha kikundi hicho ili kwenda kumwona Rais  Kikwete kumweleza tatizo la ajira linalowakabili.
 
“Vijana hawa wanadai kuwa waliahidiwa kupewa ajira za kudumu mara baada ya kumaliza mafunzo yao ya JKT.
 
" Jambo hili sio la kweli, kwani tumefanya uchunguzi na kubaini hakuna mkataba wowote unaosema wakimaliza mafunzo lazima waajiriwe, bali kila mtu anatakiwa kutumia ujuzi alioupata kujiajiri.  
 
"Lakini walipokaa kwa muda mrefu  bila kuona ahadi yao inatekelezwa, wakaamua kuanzisha kikundi chao ambacho sio halali kwa mujibu wa sheria za nchi.
 
"Hadi sasa tumeandaa jalada la mashitaka na tumelikabidhi kwa mwanasheria wa serikali kwa ajili ya kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hawa kujibu mashitaka yanayowakabili,” aliongeza Kova katika taarifa yake.
 
Alitaja vijana wanaoshikiliwa na Polisi kuwa ni Mwenyekiti wa kikundi hicho George Mgoba (28) mkazi wa Mabibo Loyola, Katibu wao Linus Emmanuel (28) mkazi wa Tabata, Emmanuel Richard (28) mkazi wa Kawe, Jacob Joseph (36) mkazi wa Mabibo na Rizione Ngowi (27) mkazi wa Mtoni Mtongani.
 
Akizungumzia tuhuma za kutekwa na kuteswa kwa George Mgoba, Kova alisema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini tukio hilo kama ni la kweli na kwanini watu hao walimteka.
 
 “Tunaendelea na uchunguzi kubaini kama ni kweli kijana huyo alitekwa kama anavyodai kuwa Februari 16 alitekwa na kupatikana tarehe 19 majira ya saa  nne usiku huko Tungi Kibaha kandokando ya barabara, pia tujue ni akina nani walimteka na kwasababu zipi kisha watu hao tutawapeleka mahakamani,” alisema Kova.
 
Kova alieleza kuwa “Februari 22 mwaka huu majira ya saa kumi na moja jioni, George Mgoba alijaribu kutoroka wadini katika Hospitali ya Muhimbili lakini polisi walibaini ujanja wake na kufanikiwa kumweka kizuizini. Lengo lake ilikuwa ni kukimbia matibabu na kuzua hofu kwa wananchi”.
 
Kwa sasa Mwenyekiti huyo wa vijana hao bado amelazwa katika  Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akipatiwa matibabu. 
 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja katika Hospitali  hiyo ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha  alisema jana kuwa hali ya mtu huyo, inaendelea vizuri na afya yake imeimarika.
 
Wakati huo huo, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari baadaye jana, Kova alimtaka Makamu Mwenyekiti wa Vijana hao, Parali Kiwango (25) mkazi wa Temeke Mikoroshini ajisalimishe mara moja Polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi, kabla jeshi hilo halijaanza kumtafuta.
 
“Jeshi la Polisi linamtaka Makamu Mwenyekiti ajisalimishe mara moja kwani jana alipoona Katibu wake amekamatwa alikimbia na kutokomea kusikojulikana. 
 
"Yeye kama ni mhitimu wa JKT hatakiwi kukimbia, bali ajisalimishe mwenyewe katika ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Polisi Kanda  Maalumu Dar es Salaam au kituo chochote cha Polisi kilicho karibu na alipo,” aliongeza Kova.

Mwanajeshi Mwingine wa JKT ambaye ni Katibu wa Vijana wa JTK Waliotaka Kuandamana Akamatwa Akituhumiwa Kufanya Mkusanyiko Usio Halali



KATIBU wa vijana waliopata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) waliokuwa wakiandamana kushinikiza Serikali kuwapatia ajira, Rinus Emmanuel amekamatwa jijini Dar es Salaam.
 
Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wao George Mgoba, kutekwa wiki iliyopita na kisha kupigwa na kuteswa na watu wasiojulikana.
 
Hata hivyo Mgoba alihamishwa kutoka Hospitali ya Amana, Ilala na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), ambapo anaendelea kupata mateso kutokana na kutopatiwa matibabu katika hospitali hiyo.
 
Katibu huyo alikamatwa jana akiwa na wenzake wawili wakati wakiwaongoza wenzao kwenda kumwona mwenyekiti wao, aliyelazwa katika Hospitali ya Muhimbili.
 
Akizungumza na Mpekuzi jana, Msemaji wa vijana hao, Omary Bakari alisema katibu wao alichukuliwa ghafla na polisi walipokuwa wanaingia eneo la Muhimbili muda mchache baada ya kushuka kwenye gari.
 
“Hatujui nini kinaendelea hadi sasa na kwa nini polisi wanatufanyia vitendo hivi wakijua sisi si wahalifu, tunasikitika sana kwa haya yanayoendelea kufanyika juu yetu,” alisema Bakari.
 
Alisema pamoja na kukamatawa kwa katibu wao na watu waliodai ni askari polisi wamefuatilia kwa vyombo vinavyohusika ikiwemo polisi lakini wamekuwa wakipewa majibu ya kukatisha tama, jambo ambalo linawafanya waingiwe na hofu kuhusu hatima ya kiongozi wao.
 
Zaidi ya vijana 300 walikuwa wakiingia hopitalini hapo , huku baadhi yao wakiwa nyuma ghafla walishuka askari wakiwa wamevaa kiraia ambao walimvamia katibu wao na kuingia nae katika gari na kutokomea naye kusikojulina.
 
Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa vijana hao, Kiwango Mpalare, alisema kabla ya kwenda Muhimbili walikuwa na kikao chao katika Ukumbi wa Msimbazi Centre ambapo pamoja na mambo mengine walijadili hatima ya kumuuguza kiongozi wao.
 
“Baada ya kikao wote tulitoka na kuazimia kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili kwa lengo la kumjulia hali kiongozi wetu.
 
“Baada ya kufika hospitali tukiwa zaidi ya vijana 300 walikuja askari wakiwa katika gari na kumkamata katibu wetu kwa kosa la kukusanyika kinyume cha sheria. Tunajiuliza wapi tumekusanyika hali ya kuwa tulikuwa kwenye ukumbi wa mikutano.
 
“… je hata katika ukumbi wa mikutano napo kunahitajika kibali cha polisi, baada ya taarifa hiyo tulifuatilia polisi na kuambiwa kuwa waende wanasheria kwa ajili ya dhamana. Lakini ilishindika na wote wapo Kituo cha Polisi Cetral,” alisema Maparale.
 
Mwandishi  alipomtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kiliposi Ilala, Mary Nzuki ili kupata ufafanuzi kuhusu kukamatwa kwa vijana hao alipokea simu na alipoulizwa swali aliikata.
 
Hata alipopigiwa kwa mara nyingine zaidi ya mara tatu simu yake iliita bila kupokelewa.
 
Kutokana na tukio hilo alipotafutwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salam, Kamishna Suleiman Kova, alisema bado hajapata taarifa za kukamatwa kwa vijana hao ambapo aliomba afanye uchunguzi wa kina na taarifa atatoa leo.
 
Wiki iliyopita kiongozi wa vijana hao, Mgoba alitekwa na kisha kuteswa na watu ambao hawajajulikana, alihamishiwa katika Hospitali ya Muhimbili Ijumaa jioni akitokea Hospitali ya Amana alikokuwa amelazwa awali.
 
Mpekuzi  lilifika Muhimbili jana ikiambata na vijana hao hadi  wodi namba sita jengo la Mwaisela na kumkuta Mgoba amelazwa huku akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ambao walikuwa wamevalia nguo za kiraia.
Mwenyekiti wa JKT, George Mgoba akiwa wodini.
Baadhi ya askari wa JKT wakiwasili Muhimbili.
 Askari  Wakiimarisha  Ulinzi  eneo  la  Hospitali  ya  Muhimbili

Sunday, February 22, 2015

KWA MARA NYINGINE TENA CHADEMA WILAYANI ILEJE



TUNAKUTANGAZIA MKUTANO MKUBWA WA HADHARA UTAKAOFANYIKA TAREHE 25.2.2015 KATIKA KATA YA MALANGALI KIJIJI CHA MALANGALI, AMBAPO PAMOJA NA WATU WENGINE MKUTANO UTAHUTUBIWA NA:- 1.JOSEPH SICHEMBE alias CHINA-M.kiti CHADEMA MKOA WA MBEYA 2.GWAMAKA MBUGHI alias KAGHOMBE-KATIBU BAVICHA MBEYA 3.JAMES KAYINGA-MJUMBE KAMATI TENDAJI ILEJE.N.K HODI MALANGALI. Na njoo ujue kuhusu.

1.Msimamo wa CHADEMA kuhusu mchakato wa Latina
2.Daftari la kudumu la wapiga kura.
3.Hali ya kisiasa na uchumi
ILEJE. CHADEMA TUMAINI LETU.
Imetolewa na Gwamaka Mbughi. Kny:Katibu Mkoa-Mbeya.










Saturday, February 21, 2015

Kiongozi wa vijana JKT atekwa, aokotwa

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu 


Kwa ufupi
Si Jeshi la Polisi mkoani Pwani wala Dar es Salaam lililokuwa tayari kuzungumzia tukio la kijana huyo kutekwa, kupigwa na kutekelezwa kwenye msitu huo, lakini msemaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) alithibitisha kuwapo kwa kijana huyo hospitalini hapo kuanzia jana saa 10:30 jioni, ingawa hakutaka kutoa maelezo mengi.
Dar es Salaam. Utata umezingira suala la kijana George Mgoba, ambaye amekuwa akijitambulisha kuwa kiongozi wa wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) baada ya habari kuwa alitekwa na baadaye kutupwa kwenye Msitu wa Pugu, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Si Jeshi la Polisi mkoani Pwani wala Dar es Salaam lililokuwa tayari kuzungumzia tukio la kijana huyo kutekwa, kupigwa na kutekelezwa kwenye msitu huo, lakini msemaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) alithibitisha kuwapo kwa kijana huyo hospitalini hapo kuanzia jana saa 10:30 jioni, ingawa hakutaka kutoa maelezo mengi.
Mgoba amekuwa akihamasisha vijana wenzake waliohitimu ya JKT kukusanyika jijini Dar es Salaam na kuandamana hadi kwa Rais ili kumweleza masikitiko yao ya kutopatiwa ajira baada ya kumaliza mafunzo kama walivyoahidiwa wakati wakienda kwenye kambi za jeshi hilo.
“Ndio aliletwa hapa majira ya saa 10:30 akitokea Hospitali ya Amana,” alisema ofisa uhusiano wa MHN, Aminiel Aligaeshi.
“Lakini waganga walipotaka kumtibu alikataa kwa sharti kwamba atibiwe wakati ndugu zake wakiwapo. Ndugu zake walipofuatwa nje, hawakuonekana. Anaonekana ana maumivu sehemu ya mgongoni na anapumua kwa shida.”
Habari zinasema kuwa kuanzia saa 1:00 jioni madaktari walikuwa wakijaribu kumshauri akubali kutibiwa, lakini akakataa na hivyo kuwalazimu madaktari kumtaka asaini fomu ya kukataa matibabu. Hata hivyo hadi saa 2:00 usiku hakuwa amesaini.
Kijana huyo anasemekana kutekwa juzi jioni na watu ambao hawajajulikana na aliokotwa na msamaria mwema ambaye baadaye aliungana na watu wengine kumpeleka Hospitali ya Tumbi.
Hata hivyo, aligoma kutibiwa kwenye hospitali hiyo akitaka ndugu zake wawepo.
Habari zinasema baadaye alisafirishwa kuhamishiwa Hospitali ya Amana kabla ya kuhamishwa tena na kwenda Muhimbili jana saa 9:00 alasiri.
Mfanyakazi mmoja wa Hospitali ya Amana aliiambia gazeti hili kuwa kabla ya askari wa Jeshi la Polisi kumfuata na gari mbili aina ya Land Rover, kundi la vijana wanaosadikiwa kuwa ni wahitimu wa mafunzo ya JKT, liliwasili Amana na kutaka kushinikiza kumchukua Mgoba, lakini uongozi uliwakatalia kwa maelezo kuwa wangetoa ruhusa hiyo kama wangekuwapo ndugu zake.
Alivyotekwa
Mwandishi wetu kutoka Kibaha anaripoti kuwa kijana huyo, anayejielezea kuwa ni mtetezi wa vijana waliohitimu JKT, aliokotwa kwenye kichaka kilichopo Picha ya Ndege mjini humo akiwa amejeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwilini.

Thursday, February 19, 2015

LORI LA MAFUTA LAUA NA KUJERUHI TENA MBEYA


WATU WAWILI 1. MARIA PAJELA [18] NA 2. WILLIAM S/O PASCHAL [38] ,WOTE WAKAZI WA KIJIJI  CHA IDWELI, KATA YA ISONGOLE, TARAFA YA UKUKWE WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA, WALIFARIKI DUNIA BAADA YA KUUNGUA MOTO KIJIJINI HAPO JANA.


TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI LEO, IMESEMA KUWA, KATIKA TUKIO HILO MAREHEMU HAO PAMOJA NA BAADHI  YA WANANCHI WENGINE WA KIJIJI HICHO WALIKUWA KATIKA HARAKATI ZA KUIBA MAFUTA KUTOKA KATIKA GARI T.891 AQZ /T.821 ARF AINA YA SCANIA MALI YA AILIS SANGA LILILOKUWA LIMEBEBA MAFUTA AINA YA PETROLI UJAZO WA LITA 41,000, LIKITOKEA DSM KUELEKEA NCHINI MALAWI,  LIKIENDESHWA NA DEREVA ZAWADI NYATO [46] MKAZI WA SAE MBEYA AKIWA NA TINGO WAKE FRANK YOHANA [24],MKAZI WA MBOZI.

AWALI KABLA YA TUKIO HILO GARI HILO LILIACHA NJIA NA KUPINDUKA, HIVYO WAHANGA [DEREVA NA TINGO] WALIFANIKIWA KUOKOLEWA NA KUPELEKWA KITUO CHA POLISI KIWIRA ILI KUPATA HATI YA MATIBABU [PF3] KWA AJILI YA KWENDA HOSPITALINI KUPATIWA MATIBABU. HATA HIVYO BAADHI YA WANANCHI WA ENEO HILO WALIVAMIA GARI HILO NA KUFANIKIWA KUTOBOA TANKI LA MAFUTA, HALI ILIYOPELEKEA MAFUTA KUANZA KUMWAGIKA/KUSAMBAA MAENEO HAYO NA HATA KUELEKEA MAENEO YENYE MAKAZI YA WATU  NA WAO KUKINGA KWA KUTUMIA VYOMBO VYAO.


KATIKA TUKIO HILO WATU KUMI NA NANE [18] WALIJERUHIWA, KATI YAO WANAUME NI 13 NA WANAWAKE 05 AMBAO NI: 1. SHUKURU KANZALE [21], 2. NURU GEORGE [30], 3.ASANTE BONIFACE [38], 4. JOSEPH JAMSON [18], 5.JOSEPH PASCHAL [30], 6.SIZA KANESA [22], 7.ALEX  DAUD [35], 8. OSCAR YOSIA [23], 9.TRAIPHON MOASI [37], 10.SAMSON MBWILA [29].

WENGINE NI 11. DORA MICHAEL [35],12. VERONICA ELIA [30],13.RABSEN AYUB [26], 14.WASIWASI SPIKA [32], 15.ASIA ANON [20], 16.BAHATI KYANDO [23], 17. CHRISTOPHER ERASTO [32] NA 18. MELISA SANANE [50], WOTE WAKAZI WA KIJIJI CHA IDWELI. AIDHA KATI YA MAJERUHI HAO,MAJERUHI 16 WAMELAZWA HOSPITALI YA MISHENI –IGOGWE NA MAJERUHI WAWILI WAMELAZWA HOSPITALI YA SERIKALI MAKANDANA-TUKUYU NA HALI ZAO ZINAENDELEA VIZURI.

Wednesday, February 18, 2015

Wapiganaji 300 wa Boko Haram wauawa

  jeshi la Nigeria limesema kuwa limewauwa zaidi ya wapiganaji 300 wa Boko Haram, baada ya jeshi la nchi hiyo kutwaa tena miji kadhaa iliyotekwa na wapiganaji hao kazkazini mashariki mwa Monguno.
Msemaji wa jeshi Chris Olukolade amesema kuwa wapiganaji wachache wa kiislamu pia wamekamatwa.
Bado hakujatolewa taarifa zaidi kuthibitisha habari hizo.
Mataifa kadhaa ya magharibi mwa Afrika kama vile Niger, Chad na Cameroon, ambayo yanakabiliana na Boko Haram pia yametoa taarifa ya maafa makubwa kwa kundi hilo ambalo limeleta kero kubwa katika ukanda huo.
Siku ya jumatatu wiki hii jeshi la Nigeria lilisema kuwa limeutwaa tena mji wa Monguno, ambao ulikuwa umetekwa na wapiganaji hao wa jihadi mwezi uliopita.

Tuesday, February 17, 2015

MAGARI YAKWAMA KWA ZAIDI YA MASAA MAWILI ENEO LA NANE NANE BAADA YA MTI MKUBWA KUANGUSHIWA BARABARANI.


Magari makubwa yakiwa yamesimama kusubiri miti kuondolewa barabarani katika eneo la Nanenane jijini Mbeya.
Vibarua wakihangaika kuondoa miti iliyoangukia barabarani baada ya kuangusha mti katika shamba la Chuo cha Kiliomo Uyole.
Baadhi ya Vibarua wakiwasaidia waliokata miti kuondoa barabarani ili kupisha magari kuendelea kupita.
Barabara ikionekana kufungwa bila kuwepo kwa tahadhari yoyote.
Miti ikiwa imeziba Barabara.




Baadhi ya magari yakiwa kwenye foleni yakisubiri miti kuondolewa barabarani.

MAGARI yanayotumia barabara kuu ya TANZAM  yamekwama kwa zaidi ya masaa mawili katika eneo la Nanenane jijini Mbeya  baada ya mti mkubwa kuangushiwa barabarani.
Mti huo mkubwa umekatwa na watu ambao hawakufahamika majina yao mapema ambapo walishindwa kuuzuia na kuangukua kwenye barabara hiyo na kusababisha usumbufu kwa watumiaji wa barabara hiyo.
Hata hivyo watu hao hawakuweka tahadhari ya aina yoyote wakati zoezi hilo likiendelea jambo lililosababisha baadhi ya madereva wa magari madogo na magari ya abiria kulazimika kuchepuka na kupita barabara zingine ili kuwahi muda.
Aidha hakuna Askari wa usalama barabarani aliyeweza kugundua hali hiyo huku baadhi ya Madereva wa magari makubwa wakilaani kitendo hicho kuwa ni kushindwa kuheshimu matumizi ya barabara na watumiaji wengine.