VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Friday, January 30, 2015

Auwawa na mwiliwake kutundikwa juu ya mti soma zaidi hapa

WATU wawili wameuawa katika matukio tofauti, akiwemo kijana mmoja ambaye hajafahamika jina wala makazi yake. 

Kijana huyo alikutwa amenyongwa na watu wasiofahamika kisha mwili wake kutundikwa juu ya mti kwa kutumia suruali aliyokuwa amevaa katika kijiji cha Ibadakuli, Manispaa ya Shinyanga.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Longinus Tibishubwamu alisema tukio hilo limetokea Januari 27, mwaka huu. Alisema mwili ulikutwa na jeraha kwenye mguu wa kulia na uchunguzi wa daktari unaonesha kuwa kijana huyo aliumia kabla ya kunyongwa shingo na chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana.

Wakati huo huo, Kamanda Tibishubwamu alisema mwanamke asiyefahamika jina wala makazi yake anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30 ameuawa kisha mwili wake kuwekwa chini ya daraja dogo lililopo katika kitongoji cha Jihingu kata ya Kolandoto manispaa ya Shinyanga.

Aliongeza kuwa mwili wa marehemu umekutwa ukiwa na majeraha kichwani, usoni na ubavuni na kwamba Jeshi la Polisi linafanya uchunguzi juu ya mauaji hayo ili kuwabaini na kuwakamata wahusika.

Thursday, January 29, 2015

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO. BAVICHA WILAYA YA YA ILEJE. TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI KUFUATIA UHAMISHO WA MSNYANYASO NA KINYUME CHA SHERIA KWA WATUMISHI WA UMMA.





Taarifa hii ni maalumu kwa umma na vyombo vya habari kwa kukemea,kulaani na kupinga vikali vitendo vya uonevu na unyanyasaji kwa watumishi wa umma hususani walimu ILEJE wanao unga mkono harakati za mageuzi ya kisiasa kupitia CHADEMA na washirika wake ie UKAWA.Uonevu na unyanyasaji huu unafanywa na baadhi ya mamlaka za Kiserikali kwa ushirika na CCM kwa kukiuka waziwazi katiba,sheria na kanuni zote zinazo husu utumishi wa summa (shinikizo toka CCM kufuatia katibio la anguko lake)


Ndugu Wananchi,CHADEMA kupitia BAVICHA tunaomba ifahamike kuwa hakuna sheria yeyote katika vitabu vya sheria inayokataza watumishi wa umma hususani walimu ama watumishi wengineo isipokuwa baadhi ya makundi kujihusisha na siasa ama za upinzani au chama tawala katika kipindi husika.,Na hakuna sheria ama kanuni inayoelekeza ama kulazimisha watumishi wa umma kuwa wapambe,wakereketwa,mashabiki ama wanachama wa chama tawala tu yaani CCM isupokuwa upinzani.

Ibara ya 20(1) ya katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania inaelekeza kuwa "Kila mtu anao Uhuru wa kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani ,kuchanganyika,kushirikiana na watu wengine na kwaajili hiyo kutoa mawazo yake hadharani na kuanzisha na kujiunga vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kubifadhi au kuendeleza inami au maslahi yake au maslahi ya wengine"

Ibara ya 20(4) ya Katiba hiyo hiyo inaeleza kuwa "Itakuwa ni marufuku kw mtu yeyote kulazimishwa kujiunga na chama chochote au shirika lolote au kwa chama chochote cha siasa kukataliwa kusajiliwa kwasababu tu ya itikadi au falsafa ya chama hicho".Rejea pia Uhuru wa MTU kushirikiana na wengine sheria ya 1984 Name.15 in 6, she ria ya 2005 Na 1 ib 7.

Kwa kuzingatia vifungu hivyo vya katiba na sheria si shaka kuwa hakuna Mwalimu anayekayazwa kuwa CHADEMA kwani hata sheria nakanuni zinzotokana na katiba hazikatazi.Kwa mujibu wa kanuni za maadili ya utendaji wa utumishi wa umma toleo la 1998 kanuni namba 9(1) inaeleza kuwa KILA MTUMISHI ANAYO HAKI YA KUSHIRIKI MASUALA YA SIASA,na toleo la mwaka 2005 kanuni namba 5 (1&2) inaeleza kuwa WATUMUSHI WANAYO HAKI YA KIDEMOKRASIA KUSHIRIKI MASUALA YA SIASA NA KUWA NA VYAMA.

Hivyo kwa kuzingati katiba ,sheria na kanuni hizo za utumishi wa umma BAVICHA tunalaani vikali vitendo wanavyofanyiwa watumishi wa umma hususani walimu kwasababu tu ni wakereketwa,mashabiki na wanachama wa CHADEMA.

Tunalaani kitendo cha serikali kupitia Mkurugenzi wa wilaya ya ILEJE na Afisa utumishi wa wilaya kutishia kuwafukuza kazi na kuwahamisha vituo vya kazi bila kufuata sheria za utumishi wa umma mwalimu Emmanuel Mbuba aliyekuwa Ileje day,Lusekero Mwasasumbe wa Luswisi na Edgar Katembo aliyekuwa ILEJE day kwa Kile kinacho daiwa ni wafuasi wa CHADEMA. Na kama hiyo haitoshi wamewahamisha vituo vyao vya kazi pasipo kuzingatia kanuni za utumishi wa umma ambazo zinaelekeza kuwa uhamisho ufanyike Mara baada ya mtumishi kuhudumu kituo chake kwa muda wa miaka mitatu (3) lakini imekuwa kinyume kwa watumishi hawa kwani wamehamishwa kwa shinikizo la kisiasa toka CCM. Ifahamike kuwa hata kama ni wafuasi wa CHADEMA hawakupaswa kupewa kile kinacho itwa uhamisho wa kukomoa kwani hakuna sheria inayo kataza wao kuwa CHADEMA.

BAVICHA tunatambua kuwa pasipo chembe ya hofu wala shaka ,kuwa kitendo hiki ni shinikizo la CCM kwani historia inaonesha 1/8/2013 Mkurugenzi wa wilaya wakati huo alipewa shinikizo na Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi CCM Taifa Abdah Bulembo la kutoa uhamisho wa kukomoa kwa Mwalimu Bahati Nkota kwa Kile kilichoitwa yupo CHADEMA na si vinginevyo. Ikiwa ni mwendelezo ule ule tunatambua kuwa uhamisho wa na vitisho kwa mwalimu Emmanuel Mbuba,Edgar na wengineo unatokana na maazimio ya kikao cha CCM kilichofanyika Mbeya novemba 2014 ambapo kilihudhuliwa na Mkurugenzi ILEJE, Mkuu wa Mkoa, Aliko Kibona (MB) na makaada wengine waaminifu wa CCM ILEJE ambapo pamoja na mambo mengine kilijadili kuwashughurikia kwa namna yeyote ile watumishi wote hususani walimu wote wanao unga mkono upinzani kwa namna yeyote ile.

BAVICHA tunahoji, kama kweli sheria inakataza watumishi kushiriki siasa inakuaje kwa walimu Wito Mlemelwa, Said Ngondo wa Lubanda,Magelanga wa Mkumbukwa,Yoloda Kilonge wa Lubanda,Simbeye wa Nakalulu na Sanga wa Ilulu ambao ni makaada watiifu wa CCM mbona hawapewi kalipio? Au ni kwa CHADEMA tu?

BAVICHA tunamtaka Mkurugenzi akome Mara moja kutumika na CCM ili kukandamiza upinzani kwani kwa namna yeyote ile hayoweza kuzuia mabadiliko haya ya kisiasa wilayani ILEJE kwani ni kama mafuriko hivyo hatoweza kuzuia kwa mikono ama namna yeyote ile, YASIJE MZOA PIA.

Pia tunakishauri chama cha walimu ILEJE (CWT) kukemea kwa vitendo manyanyaso na uonevu wa aina yeyote unaofanywa kwa wanachama wake kwani wamekuwa wakichangia michango na gharama za uendeshaji wa CWT hivyo ni vema umoja huu ukatimiza wajibu wake pia kwa kuwalinda wanachama wake pindi wanapo kandamizwa.

MUHIMU: tunataka Mkurugenzi na makundi mengine watambue kuwa BAVICHA hatupingi kuhamishwa vituo vya kazi watumishi wa umma Bali tunataka uhamisho uwe wenye haki kwa kuzingatia sheria na kanuni za utumishi wa umma na si shinikizo toka CCM.

Imetolewa na Gwamaka Mbughi.
M/kiti BAVICHA ILEJE.
+255 764 107 610..

Nakala kwa Mkurugenzi
Nakala CWT ILEJE.

Wednesday, January 28, 2015

ZIARA YA MBUNGE JOSEPH MBILINYI ( SUGU) ILIYOFANYIKA WILAYANI ILEJE


 Mh: joseph mbilinyi akicheza ngoma ya  asili na wananchi


 Picha ikimuonyesha mh: joseph mbilinyi akiwa jukwani akiwahutubia mamia ya watu wilayani ileje

             picha na
                                                vitus mtafya



























Tuesday, January 27, 2015

CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA RUNGWE KIMEINGIA KATIKA KASFA NZITO BAADA YA KUDAIWA KUUTEKA MSAFARA WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) NA KUWAJERUHI KWA MAPANGA,MARUNGU NA NONDO.





 Ndg. Max Mwasomola ni Mmoja wa waliojeruhiwa aliyeng'olewa jino na kukatwa kucha
 
 Mwenyekiti wa BAVICHA taifa Ndg. Patrick Ole Sosopi akimtakia hali Max Mwasomola aliyeng'olewa jino na kukatwa kucha na viongozi wa CCM.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Rungwe Mbeya kimeingia katika kashfa nzito baada ya kudaiwa kuuteka msafara wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  kuwatesa na kuwajeruhi kwa mapanga,rungu na nondo huku wakiwang’oa meno na kucha viongozi watatu wa chadema.
Akizungumza na Tanzania daima leo (jana) kamanda wa ulinzi na usalama wa jimbo la Rungwe Magharibi Reonad Joseph alisema tukio hilo lilitokea saa moja usiku wa kuamkia leo wakiwa njiani wakitokea kata ya Lufilyo walikokuwa wakifanya mkutano.
Alisema Chadema ilikuwa kwenye ziara wilayani humo ambayo iliongozwa na naibu mwenyekiti wa baraza la vijana (BAVICHA) huku Chama cha Mapinduzi wakifanya ziara iliyokuwa chini ya mwenyekiti wao wa mkoa wa Mbeya…… na kwamba wananchi walikuwa mwakisusia mikutano yao na kujaa katika mikutano ya Chadema.
Kutokana na hali hiyo Chama Cha Mapinduzi kupitia makada wake walipanda kuuteka msafara wa viongozi wa Chadema wakati wa kurejea Tukuyu mjini maeneo ya kata ya Mbambo walilazimika kubadirisha njia ili kuwanusuru viongozi wa kitaifa na hatimaye wakafanikiwa kuwateka viongozi watatu waliokuwa na pikipiki.
Aliongeza kuwa baada ya kuwateka viongozi hao walianza kuwapiga na kufanikiwa kuwakata na mapanga maeneo mbalimbali ya sehemu za mwili wao na kuwang’oa meno na kucha  ambapo walikuja okolewa na wananchi wa eneo hilo na hatimaye kuwakimbiza katika hospitali ya wilaya kwa matibabu na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi wilayani humo.
Katibu wa siasa itikadi na uenezi wa jimbo hilo,Grece Kalambo alishangazwa na hatua ya Chama hicho kuendesha operesheni hiyo,na kuwa siasa sio ugomvi wanatakiwa kushindana kwa hoja na si kuleta vita pamoja na kuwa wananchi tayari wamekichoka chama hicho wanatakiwa kujitathmini upya.
Mwenyekiti wa jimbo hilo,Juma Kibo alisema chanzo cha Chama hicho kuendesha utekaji kwa viongozi wa chadema ni kutokana na wananchi kususia mikutano yao na kujaa kwenye mikutano ya Chadema kutokana na kuwa na maelezo na sera nzuri zinazowavutia wananchi kila kona.
Kibo aliwataja baadhi ya viongozi waliotekwa na kuteswa kwa kukatwa na mapanga,kung’olewa meno na kucha ni mwenyekiti wa bavicha wilaya,Gastor Mwakasege,aliyepigwa lungu begani na kupokonywa pesa Tsh,laki 2.9 pamoja na simu,Jonathani Mwakyusa aliyekatwa mguu na kupokonywa viatu vyenye thamani ta Tsh,30,000,na Max Mwasomora aliyeng’lewa jino na kucha.
Makamo mwenyekiti wa Baraza la vijana (BAVICHA)Taifa Patrick Olle Sosopi mbali na kushangazwa na tukio hilo alisema utekaji huo ulimlenga yeye na kuwa anaipongeza kamati ya ulinzi na usalama wa jimbo hilo kwa kutambuo hilo na kunibadirishia njia.
Kutokana na hali hiyo Sosopi alilishutumu jeshi la polisi wilayani humo kwa kutowapa ulinzi baada ya kuwapa taarifa juu ya uwepo wa utekaji huo na kwamba majeruhi walipelekwa hospitalini na kwamba wamefungua jarada la kesi nambaTUK/IR/115/2015 shambulio na faili la kesi ni CC NO-9/2015.
Sosopi alisem wameliachia Jeshi la polisi lifanye kazi yake na kuwa kama kutakuwa na upendeleo kwa Chama cha mapinduzi basi watatoa maamuzi magumu juu ya wahusika wote kwa kuwa CCM inakila kitu lakini Chadema wanategemea nguvu ya umma,’’kwa sasa tunaendelea na ziara katika maeneo yote tuliyoyapanga’’alisema.
Mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) wilayani humo,Arbat Kawonga mbali na kukili kuwepo na tukio hilo alisema Chama chake hakihusiki na tukio hilo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilayani humo,Ally Mwakalendile alisema yeye hakuwepo wakati tukio hilo likitokea na kuwa hawezi kuzungumza chochote.
Jeshi la polisi wilayani humo limekiri kuepo na tukio hilo na kuwa tayari linamshikilia dereva wa gari aina ya Noah lenye namba T,408 DBM lililotumika kwa shughuri hiyo na kwamba dereva wa gari hilo amepelekwa mahakamani leo na kufunguliwa shitaka hilo.
Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya hiyo Dkt,Sungwa Ndagambwe amekiri kupokea majeruhi hao na kuwa wanaendelea kupatiwa matibabu na hali zao zinaendelea vizuri.
Mwisho.

Monday, January 26, 2015

TRA YATOA SEMINA YA HIMAYA MOJA YA FORODHA KWA TUME YA MIPANGO


Mtaalamu wa Masuala ya Forodha kutoka TRA, Bw. Stambuli Myovela (Kulia) akizungumza wakati wa Semina ya Himaya Moja ya Forodha (Single Customs Territory) kwa watumishi wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.
Baadhi ya watumishi wataalamu wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakifuatilia kwa umakini mawasilisho kuhusu Himaya Moja ya Forodha (Single Customs Territory) katika semina iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).

Na Saidi Mkabakuli

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imetoa semina juu ya Himaya Moja ya Forodha (Single Customs Territory) kwa watumishi na viongozi waandamizi wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango.

Akizungumza katika ufunguzi wa Semina hiyo, Naibu Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango na Mkuu wa Kongane ya Biashara ya Kimataifa na Ushirikiano wa Kiuchumi, Bw. Paul Sangawe amesema kuwa semina hiyo ina lengo la kuhakikisha kuwa kuna uelewa wa pamoja kuhusu utaratibu huo kwa watumishi wa umma na watanzania wote.

“Lengo la semina hii ni kupata ufahamu wa kutosha kuhusu mambo mbalimbali yanayoendelea, ili kuweza kushauri Serikali ipasavyo katika masuala mbalimbali ya kisera katika Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki,” alisema Bw. Sangawe.

Akiwasilisha mada juu ya Mfumo wa Himaya Moja ya Forodha kwa watumishi, Mtaalamu wa Masuala ya Forodha, Bw. Stambuli Myovela alisema kwamba mfumo huo unaainisha utaratibu wa Mzunguko Huru wa Biashara, Usimamizi wa Mapato, na Mfumo wa Kisheria. 

Bw. Myovela aliongeza kuwa kwa mujibu ya mfumo uliokubalika ni kwa kila Nchi Wanachama zitakushanya mapato yake ya kodi. Aidha, kwa bidhaa zinazopitia Nchi moja kuelekea katika Nchi nyingine wanachama (Transit Goods), Nchi Wanachama zimekubaliana kuwa nchi husika bidhaa zinapokwenda itakusanya mapato yake na kuifahamisha mamlaka ya forodha mizigo ilipoingilia katika Jumuiya kwa ajili ya kuruhusu bidhaa kuondoshwa. 

Akieleza namna ya utendaji kazi wa mfumo huo, Bw. Myovela aliongeza: “Baada ya kuthibitisha kuwa kodi imelipwa, mizigo itasafirishwa kutoka kituo cha kwanza cha forodha chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Forodha kwenda nchi ambayo mizigo hiyo imekusudiwa kutumika ndani ya Jumuiya. Mfumo maalum wa ufuatiliaji kielektroniki (Electronic Cargo Tracking System) utatumika kuhakikisha mizigo inafika salama katika nchi iliyokusudiwa katika Jumuiya.”

Mfumo wa Himaya Moja ya forodha uliridhiwa na Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Mkutano wake wa 28 ambapo kwa pamoja Mawaziri hao waliridhia kuwa na Mpangokazi unaoainisha masuala ya kutekeleza katika kipindi cha miezi sita ili kuwezesha kuanzishwa kwa Himaya Moja ya Forodha ifikapo mweizi Juni, 2014.

Mabadiliko ya Mawaziri


        Mawaziri wawili wamejiuzulu
    
  i) Ardhi-Tibaijuka
 
ii)Nishati na madini-Sospeter Muhongo
Walio teuliwa
 
1. George Simbachawene- Waziri Nishati
 
2.Mary Nagu-Waziri wa Nchi mawasiliano na Uratibu
3.Christopher Chiza-Waziri uwezeshaji na Uwekezaji
 
4.Halson Mwakyembe-Ushirikiano wa afrika mashariki
 
5.Lukuvi-Ardhi Nyumba na Makazi
 
6.Steven Wasira-Kilimo chakula na Ushirika
 
7.Samwel Sitta -Wizara ya Uchukuzi
 
8.Jenista Muhagama-Sera na uratibu wa Bunge

 
MANAIBU Waziri
 
Masele -OMR Muungano
 
Kairuki -  Ardhi
 
Ummy - Katiba na Sheria
 
Anna Kilango- Elimu
 
Mwijage - Nishati

Friday, January 23, 2015

WALIMU MBEYA WALIPOANDAMANA KUDAI HAKI ZAO. WAMUOMBA RWEGAMALILA AWASAIDIE


 Walimu Jiji la Mbeya, wakiwa wamezuiwa na FFU ili wasiendelee kuelekea ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya.

WALIMU wa shule za Msingi na Sekondari katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, wapatao 113, juzi waliandamana kuelekea ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji hilo kwa ajili ya kudai haki zao mbalimbali.

Maandamano hayo ya amani, yalianzia katika ofisi kuu ya Jengo la CWT Mkoa wa Mbeya majira ya saa 5;27 asubuhi, kabla hayajazuiwa na kikosi cha askari wa kutuliza ghasia mkoani hapa saa 5;33 mpaka saa 5;39 na kuwaomba warejee ofisini kwao kutokana na hali ya vurugu iliyokuwa imelizingira Jiji hilo jana.

“Tunawaomba mrudi ofisini kwenu na sisi tutaenda kumleta Mkurugenzi wa Jiji, kwasababu hata mkijaribu kwenda muda huu hamtaweza kuonana naye, ulinzi umeimarishwa sana kutokana na mgomo wa wafanyabiashara wa soko la Soweto ambao wamegoma na wanataka kuandamana” alisikika mmoja wa askari mwenye nyota tatu, akiwasihi walimu hao.

Wakizungumza na waandishi wa habari, walimu hao walisema kuwa, walifikia uamuzi wa kwenda kumuona mwajiri wao kutokana na madai mbalimbali yakiwemo malimbikizo ya mishahara yao tangu mwaka 2007.

“Mwalimu unaingia darasani ukiwa na mawazo ya fedha zako huku ukiangalia dawati la mwanafunzi limechoka. Serikali inajisikia raha kuona mwalimu anaenda na biashara ya ubuyu shuleni! Mimi nadai zaidi ya Milioni Nne tangu mwaka 2007 sijalipwa na fedha tunaambiwa zimekuja zinafanya kazi zingine”alisema Mwalimu Stella Robson.

Mwalimu Lucas Mahenge, ambaye ni mlemavu wa macho, alisema kuwa yeye madai yake ni suala la kupandishwa madaraja bila kupandishwa mshahara, hali ambayo alisema inamkatisha tamaa na serikali isifikie mahala ikawafikirisha walimu kuanza kuwafundisha watoto kuwa 2+2=22.

“Serikali kama imeshindwa kutulipa madai yetu, ituambie ili tuweze kumwomba mfanyabiashara, Rwegemalil” alisema Mwalimu Gunza Mwasomola.

Katibu wa Chama cha walimu Jiji la Mbeya, Mwalimu Felix Mnyanyi, alisema kuwa kwa kushirikiana na viongozi wenzake, wamefuatilia kwa muda mrefu madai hayo na kufanya uhakiki lakini utekelezaji wake umekuwa siyo wa kuridhisha.

“Walimu wamefika hapa wakiwa na madai zaidi ya matatu, ambayo ni malimbikizo ya mishahara tangu mwaka 2007, ambapo ni wilaya pekee nchini walimu hawajalipwa, madai ya fedha za likizo, kupanda na kushushwa madaraja baada ya kujiendeleza kitaaluma na walimu wastaafu kutolipwa” alisema Mwalimu Mnyanyi.

Alisema kuwa baada ya kuzuiwa na kuwaelewa askari polisi kuwa wasifike katika ofisi ya mwajiri wao ambaye ni Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, kutokana na hali ilivyokuwa ya utata wa usalama wao na watu wengine, walirejea ofisini hapo na kuendelea kumsubiri mwajiri huyo chini ya ulinzi wa polisi, hali ambayo mpaka majira ya saa saba mchana, walimu waliendelea kuwepo katika ofisi yao na Mkurugenzi hakuweza kufika kwa wakati huo mpaka tunaenda mitamboni.

Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Mussa Zungiza, alikiri kuwepo madai ya walimu katika ofisi yake na kwamba madeni hayo hayatawezwa kumalizwa kwa siku moja kutokana na walimu kutofautiana muda wa kuanza likizo na kumaliza.
 
Alwaambia walimu kuwa atashughulikia madai yao kwa kushirikiana na uongozi wao wa CWT.

Uhamisho kwa Watumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa January 2015.




Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI inatangaza orodha ya Majina 4352 ya watumishi wa Umma waliohamishwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini Januari 2015. Aidha orodha ya watumishi 96 ambao hawakukidhi vigezo vya kuhama nayo imetangazwa.
Maelekezo yote muhimu yapo katika barua ambayo kila mtumishi atapatiwa kupitia kwa Wakurugenzi wa Mamlaka wanazotoka.


Tuesday, January 20, 2015

Mwili wa dereva wakutwa umenyongwa ndani ya gari



Mwili wa aliyekuwa dereva wa gari la mizigo Bw Ally Athumani Ally ambaye alikuwa akitafutwa na jeshi la Polisi kufuatia wizi wa milango umekutwa ndani ya gari alilokuwa anaendesha baada ya siku 4 ukiwa umenyongwa kwa kamba Wilayani Ilala.
Kamanda wa polisi mkoa wa Ilala SACPi Mary Nzuki
Mwili wa aliyekuwa dereva wa gari la mizigo Bw Ally Athumani Ally ambaye alikuwa akitafutwa na jeshi la Polisi kufuatia wizi wa milango umekutwa ndani ya gari alilokuwa anaendesha baada ya siku 4 ukiwa umenyongwa na kamba za kubebea mizigo mikubwa huku gari hilo likiwa limeegeshwa kituoni hapo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Ilala SACP Mary Nzuki amekili kutokea kwa tukio hilo ambapo baada ya watu hao kufanya mauaji hayo waliuweka mwili huo katika kitanda kilichopo katika gari hilo na kuiba mzigo wa milango uliokuwepo katika gari hilo ambao ulikuwa ukitokea bandarini kwenda katika ghala la mizigo la kampuni ya J Fogh Logistics.
Aidha katika hatua nyingine kamanda Nzuki amesema baadhi ya milango imekwisha patikana na jumla ya watu saba wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo ambapo watu hao watafikishwa mahakamani pindi uchunguzi utakapo kamilika.
Akizungumzia tukio hilo dereva mwezake na marehemu Bw Sultani Salum ambaye alifika kituoni hapo kwa ajili ya kuchukua gari hilo amesema kuwa yeye ndiye aliye gundua kuwepo kwa mwili huo baada ya kuona damu ikitokea kitandani na hivyo kulazimika kutoa taarifa ya kuwepo kwa tukio hilo.

Sunday, January 18, 2015

PROF. MWANDOSYA NA UTATU WA SIASA ZA MBEYA

Prof. Mark Mwandosya

SIASA za mkoa wa Mbeya, zina historia kubwa sana. Historia hiyo haimwachi mbali, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya kwa miaka 15, Patrick Nswilla, John Mwakangale, mzee Mwambulukutu na Waziri asiye na wizara maalum ofisi ya Rais, Prof. Mark James Mwandosya.
Kiongozi huyu ni Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki, lililopo katika Halmashauri ya Busokelo mkoani hapa.
Kwa mkoa wa Mbeya kwa wanasiasa waliopo ndani ya mfumo wa siasa za mkoa huu, yeye ndiye mwanasiasa anayeheshimika zaidi kutokana na hulka yake ya kutabasamu na watu wa rika zote na hasa kuwa mmoja ya viongozi ambao walianza kuthubutu kuwania nafasi ya rais mwaka 2005.
Baadhi ya wananchi wa mkoa wa huu, wanamwita Prof. Mwandosya Baba wa siasa za mkoa wa Mbeya.
Heshima hiyo inatokana na yeye kuwa kiongozi wa NEC mkoa wa Mbeya, ambao aliupata baada ya mchuano mkali kati yake na Kijana Thom Mwang’onda mwaka 1997,  kisha kuibuka mshindi.
Akawa kiongozi mwenye heshima kubwa kwa siasa za Mkoa wa Mbeya, kabla hajakengeuka na kujisahau kutohudhuria vikao vya chama chake, mkoa wa Mbeya.
Wakati baadhi wakiendelea kumpa heshima yake, baadhi ya waliokuwa wapambe wake mwaka huo, hawataki hata kumsikia kutokana na madai kuwa baada ya uchaguzi kuisha hakuweza kuwakumbuka hata kwa salaam na wakawa wanabezwa na kundi la Thom Mwang’onda.
Mmoja ya wapambe wa Prof. Mwandosya anayesikika mara kadhaa na kudai kuwa hajawahi kuthaminiwa baada ya ushindi ni aliyekuwa diwani wa kata ya Utengule Usongwe, Mwalimu Jackob Mwakasole, ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Kanisa la Uinjilisti Tanzania, lenye makao makuu mjini Mbalizi, wilaya ya Mbeya.
Mwingine ambaye licha ya kumkataa kwa muda mrefu, lakini kwa sasa analitangaza vema jina la Prof. Mwandosya na kuamini kuwa akiteuliwa kuwania nafasi ya Rais kupitia CCM,  atakuwa kiongozi bora, ni Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Mbeya, Bashiu Madodi.
Kwa wafuatiliaji wa masuala ya siasa kwa mkoa wa Mbeya, Prof. Mwandosya anaendelea kukumbukwa kwa umahili wake wa kusimamia na kuhakikisha miradi kadhaa inakamilika bila upendeleo, bali kwa kufuata taratibu za serikali.
Anakumbukwa kwa kusimamia kidete uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe ambao umekamilika katika wilaya ya Mbeya, Jimbo la Mbeya Vijijini.
Inaelezwa kuwa, asingekuwa Mwandosya uwanja huo wa ndege ungeenda kujengwa mikoa ya Kaskazini, ingawa haikuwa dhamira ya serikali.
Mbali na uwanja huo wa kimataifa, pia anaendelea kukumbukwa kupigania adhima ya serikali kukifanya chuo cha ufundi MIST kuwa chuo kikuu cha Sayansi na teknolojia(MUST), kilichopo Iyunga Jijini Mbeya.
Sanjari na miradi hiyo mikuu miwili, pia mradi mkubwa wa maji, ambao ulizinduliwa Julai,2012 na Rais Jakaya Kikwete, jina la uongozi uliotukuka wa Prof. Mark Mwandosya, linasadifu.
Prof. Mwandosya ni mmoja kati ya viongozi ambao wanatajwa kuwania nafasi ya rais mwaka huu, kupitia chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Rais Jakaya Kikwete, anao mtihani mkubwa katika uteuzi kama kweli ataangalia suala la urafiki. Edward Lowassa rafiki yake, Benard Membe rafiki yake, January Makamba kijana wake, Mwigulu Nchemba kijana wake, Mizengo Pinda rafiki yake na Prof. Mwandosya ni rafiki yake.
Ni mara chache ambazo Rais Kikwete amefanya ziara mkoani Mbeya bila kuambatana na Prof. Mark Mwandosya na hata katika matembezi ya sherehe za miaka 37 za CCM zilizofanyika mwaka jana 2014, mkoani Mbeya, alikuwa na Prof. Mwandosya na kiongozi huyo aliutangazia umma kuwa kwa sasa amepona na anamshukuru sana Rais Kikwete kwa kumtibu.
Kauli hiyo, ilihisiwa na wachambuzi wa masuala ya siasa kuwa ni salamu tosha kwa wawania nafasi ya rais mwaka huu 2015, ukizingatia kuwa kiongozi huyo alishika nafasi ya tatu mwaka 2005 katika mbio hizo za urais, ambapo kambi yae kubwa ilikuwa kanda ya Ziwa na sasa kambi yake imeongezeka katika kanda ya Nyanda za juu kusini.
Mbali na mapungufu ya Mwandosya kwa wanasiasa wa mkoa wa Mbeya, hasa yanayotokana na hasira za baadhi ya wapambe wake wa mwaka 1997 kwenye nafasi ya NEC, kiongozi huyu anaonekana kurejesha imani kwa kiasi kikubwa kwa baadhi ya wajumbe wa Halmashuri kuu ya Taifa waliopo mkoani Mbeya na Nyanda za juu kusini.
Wajumbe hao, awali baadhi yao walikuwa wakijinasibu kuwa ni wapiga kura watiifu wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, lakini wamebadili msimamo baada ya kile wanachodai kuwa wanaridhishwa na propaganda za kwamba wapambe wa Lowassa, wanawatembelea baadhi ya watu huku wao wakiwa wanatengwa, hivyo kuona kama kambi hiyo imejaa matapeli na hivyo ni bora kuwa wapiga kura huru.
Baadhi ya wajumbe hao, wanasema kuwa, nafasi za kura walizonazo ni tatu, hivyo moja ya kura zao itaangukia kwa Prof. Mwandosya kati ya majina matano ambayo yatapelekwa kwenye kikao chao na kamati kuu.
Baadhi ya watanzania hofu yao ni kwamba, dunia kwa sasa inapigana kuhusu suala la uchumi, je nani kati ya waliojitokeza anaweza kumudu kusimamia rasilimali za Tanzania kwa uadilifu na kukataa kuwa kibaraka wa ‘’viranja’’ wa dunia? Je ni Prof. Mark Mwandosya ataweza kutimiza adhima ya watanzania au kuendelea kuwaunganisha wananchi wa Mbeya?
Nawaasa viongozi wa CCM hasa wale wenye kura za maamuzi, kuwaletea watanzania mgombea anayeweza kuangalia uchumi wa dunia unakoelekea na namna mataifa yanavyochukua umiliki wa uendeshaji wa shughuli muhimu za kiuchumi kisha ajiulize kuwa je hii si sehemu ama aina mpya ya ujamaa?
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere angekuwepo leo hii angesemaje? Hakuna mwenye jibu sahii lakini kwa kuwa alishaonya kwenye hotuba zake, ninaloweza kuhisi ni kuwa angekumbusha kile alichowahi kusema, ambacho wengi hawakudhani kuwa kingetimia na ungekuwa wakati wa kudhihirika tena kwa maono yake.
  na makala haya inapatikana katika gazeti la MTANZANIA TAREHE 18/01/2015

Friday, January 16, 2015

SHUKRANI KWA WANANCHI WA KATA YA LUSWISI.


PICHA ZA  MKUTANO  WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO  ULIOFANYIKA KATIKA KATA YA LUSWISI  ILEJE MBEYA
      WANANCHI WAKIJIANDAA KWA MKUTANO

 KIKUNDI CHA NDOMA  KIKITUMBWIZA STEGINI




KUNDI  LA PILI NALO HIVYO HIVYO 





MATUKIO HAYA  YAMEANDALIWA  NA  :

           VITUS MTAFYA








Wednesday, January 14, 2015

Watanzania wanyongwa kwa mihadarati

Kasisi mmoja raia wa Australia amefichua na kuthibitisha kuwa kuna idadi kubwa ya wafungwa wenye asili ya Afrika katika magereza ya Hong Kong, wengi wao wakiwa ni kutoka Tanzania.


Kasisi huyo John Wortherspoon ambaye kwa sasa anafanya ziara maalum Tanzania, amesema yeye ndiye ambaye amekuwa akisambaza barua zinazodaiwa kuandikwa na wafungwa wanaoshikiliwa kwenye magereza hayo ambapo baadhi yao wametaja majina ya watu wanaodaiwa kuwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya waliowatuma kusafirisha dawa hizo.
Padre Wotherspoon amefika kuonana na familia za wafungwa hao pamoja na idara za serikali zinazohusika na mapambano dhidi ya biashara hiyo hatari ya dawa za kulevya.

Mdee: Jiandikisheni katika daftari kuepuka wizi wa kura

Wakati miezi tisa ikiwa imebaki Tanzania kufanya uchaguzi mkuu, Watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kuepuka vitendo vya wizi wa kura.

Rai hiyo ilitolewa na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, wakati akihutubia kwenye mkutano wa hadhara kwa ajili ya kuwapongeza viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Kata ya Makongo, jana jijini Dar es Salaam.

Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema Taifa (Bawacha), aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kwani kwa kutokufanya hivyo kutatoa mwanya wa kuibiwa kura na hivyo kuwapata viongozi ambao hawakuwachagua katika uchaguzi mkuu ambao unatarajiwa kufanyika nchi nzima Oktoba mwaka huu.

Alisema Tanzania siyo mali ya viongozi wa siasa bali ya Watanzania na ndiyo wenye uwezo wa kufanya mabadiliko na kwamba kura ndiyo suluhisho kubwa dhidi ya matatizo mengi yanayojitokeza nchini yakiwamo ya ufisadi wa uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow.

“Nchi hii siyo ya Mbowe, Lipumba, Mbatia au Makaidi. Nchi hii ni ya kwetu Watanzania. Wananchi ndiyo wenye wajibu wa kuibadilisha nchi hii,” alisema Mdee.

Kauli hiyo ni moja ya tahadhari kuepuka dosari ambazo zimekuwa zikijitokeza wakati chaguzi ukiwamo wa serikali za mitaa Desemba 14, mwaka jana kutokana na kujitokeza kwa idadi ndogo ya wananchi kupiga kura kutokana na kutojiandikisha katika daftari.

Aidha alieleza kutoridhishwa kwake na maamuzi yaliyotolewa dhidi ya waliohusika kwenye kashfa ya uchotwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, akisema kwamba haiwezekani watu wachote fedha hizo na kuzijaza kwenye ‘mapipa’ halafu wanaambiwa warudishe bila hatua zingine zozote.

Alisema, zaidi ya Shilingi bilioni 300 zilizochotwa kwenye akaunti hiyo ni nyingi kwani mtu anaweza kuzitumia kwa matumizi ya kawaida ya Shilingi 20,000 kila siku kwa miaka 50 ijayo.

Naye Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha), Edward Simbei, alisema, chama hicho hakitawavumilia viongozi ambao watakiuka maadili ya chama na kushindwa kuwatumikia wananchi na kujifanya miungu watu.

Sunday, January 11, 2015

DKT. SHEIN AYAPOKEA MATEMBEZI YA VIJANA WA UVCCM,ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akikagua gwaride la Chipukizi wa UVCCM wakati alipofika katika viwanja vya Mnazi Mmoja leo Mjini Zanzinar kupokea matembezi ya Umoja wa UVCCM yenye lengo la kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM wakiwa wamebeba Bendera na Picha za Viongozi wakati wa kilele cha matembezi ya Umoja wa UVCCM yenye lengo la kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyopokelewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.
Vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM wakiwa katika matembezi ya Umoja wa UVCCM yenye lengo la kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyopokelewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibarleo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekti wa CCM Zanzibar akipokea matembezi ya Vijana wa Umoja wa UVCCM yaliyofikia kilele chake leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja ikiwa ni kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Juma Khamis.
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi wakiwepo wa UVCCM wakisimama wakati Makamo Mwenyekti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea matembezi ya Vijana wa Umoja wa UVCCM yaliyofikia kilele chake leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja ikiwa ni kuadhimisha miaka 51 ya mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM wa Mkoa wa Kaskazini Unguja wakiwa katika matembezi ya Umoja wa UVCCM yenye lengo la kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyopokelewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar leo ambapo kilele chake katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akipokea picha za Viongozi kutoka kwa kiongozi wa Matembezi ya UVCCM Daudi Ismail Juma Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kupitia UVCCM wakati wa kilele cha Matembezi ya kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akimkabidhi Picha ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Juma Khamis baada ya kuyapokea matembezi ya Vijana wa UVCCM yaliyofikia kilele chake leo katika viwanja wa Mnazi Mmjoa Mjini Unguja katika kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akipokea Bendera kutoka kwa Kiongozi wa Matembezi ya UVCCM Daudi Ismail Juma Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC)kupitia UVCCM wakati wa kilele cha Matembezi ya kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.
Vijana wa Chipukizi wakipita kwa gwaride la mwendo wa haraka mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibarwakati wa kilele cha matembezi ya Umoja wa UVCCM yenye lengo la kuwaenzi Viongozi na kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar leo katika viwanja vya Mnazi mmoja mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekti wa CCM Zanzibar akimkabidhi Cheti Mke wa Makamo wa Pili wa Rais Mama Asha Suleiman kwa niaba ya Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idii kwa mchango wake mkubwa kufanikisha matembezi ya Vijana wa Umoja wa UVCCM yaliyofikia kilele chake leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja ikiwa ni kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Juma Khamis.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekti wa CCM Zanzibar akimkabidhi Cheti Makamo Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa Pili Hassan Suluhu wakati wa matembezi ya Vijana wa Umoja wa UVCCM yaliyofikia kilele chake leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja ikiwa ni kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Juma Khamis.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekti wa CCM Zanzibar akitoa hutuba yake wakati wa Kilele cha matembezi ya Vijana wa Umoja wa UVCCM yaliyofikia leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja ikiwa ni kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Juma Khamis.

Baadhi ya Vijana wa UVCCM wakimasikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pia Makamo Mwenyekti wa CCM Zanzibar alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa Kilele cha matembezi ya Vijana wa Umoja wa UVCCM yaliyofikia leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja ikiwa ni kuadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kushoto) Mwenyekiti wa UVCCM Sadifa Juma Khamis.Picha na Ikulu.