VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Monday, May 2, 2016

Prof. Lipumba Apongeza Mipango ya Rais Magufuli



Mwanasiasa mkongwe ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya uchumi nchini Profesa Ibrahimu Lipumba amesema anaunga mkono mpango wa serikali wa miaka mitano huku akisema ni vema serikali ihakikishe inawekeza zaidi katika nishati ya umeme ili kufikia lengo la kuwa nchi ya viwanda.

Wakati tayari mpango wa serikali ukiwa umekwishawasilishwa kwa miaka mitano ijayo, ambapo umeanisha namna utakavyofanikisha asilimia 40 ya ajira ifikapo mwaka 2020 zikitokana na viwanda, huku miongoni mwa miradi mikubwa uinayotarajiwa kutekelezwa ya viwanda ni ujenzi wa kiwanda cha chuma.

Aidha Mchumi huyo pia amesema adhima ya serikali ya kujenga nchi ya viwanda itafanikia ikiwa itawekeza katika nishati ya umeme wa uhakika, licha ya miradi mikubwa kama ya Power Afrika na MCC kusitishwa huku akiishauri serikali kufanyia kazi maazimio ya bunge kuhusu sakata la Tegeta esrow.

Mahojiano hayo maalum yamefanyika Dar es Salaam, muda mfupi baada ya Prof Lipumba kupokea ujumbe maalum wa wawafuasi wa chama cha CUF kutoka mjini bagamoyo waliokuwa lengo la msihi kurejea kwenye nafasi yake ya uenyekiti wa chama cha CUF.

VITUS MTAFYA ..... ILEJE NI NYUMBANI ......

No comments: