VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Wednesday, June 24, 2015

Mh: Gwamaka mbughi kutangaza nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Ileje Kupitia chama cha CHADEMA Tarehe 22/06/2015








 mkutano waKutangaza nia ya kuwania Ubunge jimbo la Ileje 2015; Mahalia:Isongole Trh:22/6/2015. ............................. SI DHAMBI KUZALIWA MASIKINI LAKINI PENGINE NI DHAMBI KUBWA SANA KUFARIKI MASIKINI KWASABA BU TU YA AMA KUTOSHIRIKI MAAMUZI YA KUPATA VIONGOZI WAZURI AU KUFANYA MAAMUZI YASIYO SAHIHI. Alisema  Mbunge Mtarajiwa kupitia chama cha CHADEMA.
maelezo mafupi kuhusu Ahadi zake kwa wananchi wa Ileje

 Ndugu zangu Wakazi wa Ileje kwa itikadi zenu nyote, Nimeisoma na kuilewa vema ibara ya 67 ib ara ndogo ya (1-13) ya katiba ya JMT 1997, ambayo pamoja na mambo mengine inaeleza SIFA,
     HAKI NA WAJIBU WA MBUNGE.Na kwa tafsiri ya jumla (yangu)ya Ibara hii inaonesha ushiriki wa Wananchi katika kumtathimini na kumpa majukumu mtu yeyote miongoni mwao kuwa Mbunge au mwakilishi kwa kuzingatia sifa tajwa. Ndugu zangu, binafsi nimejitathimini na kuja kuwashirikisha jambo na kuhitaji Baraka zenu kuwa ninao uwezo wa kuwa MBUNGE WA JIMBO LA ILEJE kwa kutimizi vema Majukumu tajwa, na hivyo natangaza kwenu rasimi kuwa nimetia nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Ileje kwa ticket ya CHADEMA, na kwamba kwa kuheshimu taratibu na kila aina ya matokeo yatakayo tokea Mara baada ya kura ya maoni kufanyika ndani ya Chama changu nitaunga mkono kwa namna nitakayo weza mabadiliko wanayohitaji Wanachi wa Ileje kwa muda mrefu sasa.

Natambua majukumu ya nafasi ninayo omba ikiwa ntapitishwa na chama changu ni pamoja.
1.Kutunga sheria
2.Kuwakilisha Wanachi
3.Kuisimamia Serikali.
  Katika majukumu hayo, hakuna sehemu inayo onesha kuwa Mbunge ni MFADHIRI ama vinginevyo kama anavyo tafsiliwi kwa RAIA wa kawaida ama kwa kuto fahamu au maksudi. CHADEMA ,tumeonesha uwezo wa kutekeleza majukumu madogo mlio tupa kupitia kwa viongozi wa serikali za mitaa mlio wachagua katika uchaguzi wa 2014 na hivyo tumieni historia hii kutuunga ama kuto tuunga mkono kwa mgombea yeyote atakaye pendekezwa miongoni mwetu Wanachadema /Ukawa kuwania Ubunge katika jimbo hili na Mimi ni miongoni mwao.

Ndugu zangu, Kila mwananchi anawajibika kwa Taifa hili; hapa tulipofika kama Taifa si kwa sababu ya watu waovu na wala rushwa, bali ni kwa sababu ya watu waadilifu na wenye hekima waliokaa pembeni na kuangalia kinachofanywa na watu waovu; Wanatumia muda mwingi kulaani giza badala ya kuwasha taa, na mtambue Kuwa serikali mbovu huchaguliwa na wasio piga kura.
Hivyo nina wasihi kuwa tujitokeze kwa wingi wakati wa kupiga muda utakapo fika ili kupata viongozi wanao tokana na matakwa yetu wenyewe na si vinginivyo. Ambapo bila kufanya hivyo tutakua tunajitakia Umasikini wenyewe.

Na ,tunaomba ifahamike kuwa CHADEMA/UKAWA hatuombi ridhaa ya miaka 50 mlio toa kwa CCM bali tunaomba ridhaa ya miaka 5 tu ambapo kupitia miaka hii mtatumia historia na kutathimini ikiwa tunafaa ama hatufai kuongezwa muda zaidi wa kutekeleza majukumu mlio tupa. Mungu awabariki na awa ongoze kupata kiongozi atakaye iunganisha Ileje,2015 na Asanteni kwa kunisikiliza"

No comments: