VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Wednesday, November 26, 2014

Makamu Rais Zimbabwe atimuliwa ZANU-PF

Makamu wa Rais wa Zimbabwe Joyce Mujuru
Vyombo vya habari vya Serikali nchini Zimbabwe vinaripoti kuwa Makamu wa Rais,Joyce Mujuru, ameondolewa kwenye kamati kuu ya chama cha ZANU-PF.
Mujuru anashutumiwa kupanga mauaji dhidi ya Rais wa nchi hiyo,Robert Mugabe.
Hatua hiyo imekuja baada ya Kampeni dhidi ya Mujuru iliyofanywa na Mke wa Rais Mugabe, Grace ambaye kwa kiasi kikubwa anaamini anataka kumrithi Mumewe atakapotoka madarakani.
Viongozi kadhaa wa ZANU-PF wameshindwa kutetea nafasi zao katika Chama hicho.
Bi Mujuru alitarajiwa kumrithi rais Mugabe mwenye umri wa miaka tisini.
Kamati ya uchaguzi katika mkoa wa kaskazini wa Mashonaland ya kati imekataa wasifu wa Makamu wa rais nchi hiyo Joice Mujuru kama baadhi ya stakabadhi zake za kuomba kazi katika uchaguzi uliofanyika siku ya Jumanne.

No comments: