VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Monday, November 17, 2014

Msako mkali dhidi ya misikiti Mombasa

Msako mkali dhidi ya misikiti Mombasa

Polisi nchini Kenya wamefanya msako mkali dhidi ya misikiti inayotoa mafunzo ya itikadi kali za kidini mjini Mombasa pwani ya Kenya.

Mtu mmoja ameuawa kwenye msako huo ulioanzishwa Jumapili dhidi ya misikiti inayosemekana kutoa mafunzo ya kuunga mkono harakati za kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab nchini Somalia.
 Misikiti ya kwanza kulengwa katika msako huo ni ile ya Masjid Musa na Sakina.

Mkuu wa polisi mjini Mombasa alinukuliwa na shirika la habari la AFP akisema kuwa walipata taarifa kwamba kundi hilo limekuwa likipanga kufanya mashambulizi na hiyo ndiyo sababu ya msako huo kuanzishwa.

No comments: