VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Sunday, December 7, 2014

IDRISS SULTAN AIBUKA KIDEDEA SHINDANO LA BIGBROTHER HUKO AFRIKA KUSINI USIKU HUU

unnamedIdriss Sultan Mtanzania aliyetikisa Bigbrother leo ameibuka mshindi wa shindano hilo na kuwabwaga washiriki kutoka mataifa mbalimbali yaliyoshiriki katika shindano hilo akiibuka na kitita cha shilingi milioni 500 za Kitanzania katika shindano hilo lililokuwa likiendelea kwa miezi mitatu nchini Afrika Kusini Idriss ni Mtanzania wa tatu kushinda shindano hilo akitanguliwa na Mwisho Mwampamba na Richard wote wakiwakilisha vizuri taifa la Tanzania katika shindano hilo, Fullshangwe inampa hongera sana Idriss kwa ushindi huo na inamtakia kila mafanikio katika maisha yake.

WAZIRI CHIKAWE ACHANGISHA ZAIDI YA MILIONI 22 KKKT JIMBO LA KASKAZINI-MAGHARIBI NACHINGWEA

unnamedWaziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akifungua zoezi la uchangiaji wa harambee ya kupatikana kwa shilingi milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa gari la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Kaskazini-Magharibi linalojumlisha Wilaya ya Nachingwea, Ruangwa na Liwale mkoani Lindi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo, anayefuata ni Katibu Mkuu wa KKKT, Dayosisi ya Kusini –Mashariki, Jane Mkimbo. Kulia ni Mkuu wa Jimbo hilo, Mchungaji Charles Mtweve. Katika harambee hiyo Shilingi Milioni 22.3 zilipatikana. Picha zote na Felix Mwagara
unnamed1Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akifungua zoezi la uchangiaji wa harambee ya kupatikana kwa shilingi milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa gari la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Kaskazini-Magharibi linalojumlisha Wilaya ya Nachingwea, Ruangwa na Liwale mkoani Lindi. Katika harambee hiyo Shilingi Milioni 22.3 zilipatikana.
unnamed2Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akitoa mchango wake wa awali shilingi milioni moja kwa ajili ya uchangiaji wa harambee ya kupatikana kwa shilingi milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa gari la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Kaskazini-Magharibi linalojumlisha Wilaya ya Nachingwea, Ruangwa na Liwale mkoani Lindi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo, anayefuata ni Katibu Mkuu wa KKKT, Dayosisi ya Kusini –Mashariki, Jane Mkimbo. Wapili kulia ni Mkuu wa Jimbo hilo, Mchungaji Charles Mtweve. Katika harambee hiyo Shilingi Milioni 22.3 zilipatikana.
unnamed3Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (watatu kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo (wanne kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Kaskazini-Magharibi, Nachingwea na KKKT Dayosisi ya Kusini-Mashariki, Kanisa Katoliki na maofisa wa wilaya hiyo, mara baada ya kumaliza harambee ya kuchangisha milioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa gari la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Kaskazini-Magharibi linalojumlisha Wilaya ya Nachingwea, Ruangwa na Liwale mkoani Lindi. Picha zote na Felix Mwagara

DIAOMOND USIPIME ANOGESHA SHEREHE YA UHURU DMV

Prezida wa Wasafi Diamond Platnumz akiwa pamoja na wacheza showa wake Roma Tonsa na Moses Iyobo wakitoa burudani katika kunogesha sherehe ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara iliyofanyika Sheraton Hotel ya Silver Spring, Maryland nchini Marekani na kuhudhuriwa na mashabiki wake kutoka kila pembe ya Marekani huku mashabiki wengine wakitokea Tanzania, Picha na Vijimabo Blog
Mzuka unazidi kupanda Diamond Platnumz asaula koti lake.
Balozi akimshukuru Diamond kwa kuwezesha kunogesha usiku wa Uhuru wa Tanzania na pia aliwashukuru wadhamini wa sherehe hiyo ya moaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Diamond akizidi kuwapa burudani mashabiki wake
Shabiki akicheza wimbo wa mdogo mdogo
Shabiki akijumuika na Diamond kwenye jukwaa.

No comments: