VITUS BENEDICTO MTAFYA

SPORT AND GAMES

Sunday, December 14, 2014

Watu kadhaa wanashikiliwa mateka Sydney

 mgahawa wa Lindt ambao tukio la utekaji limefanyika
Watu kadhaa wanashikiliwa mateka na mtu mmoja au zaidi wenye silaja katika mgahawa wa Lindt mjini Sydney, Australia.
Mamia ya Polisi waliojihami kwa silaha wamezingira eneo lilipotokea tukio hilo.
Takriban watu watatu wameonekana ndani ya mgahawa wakiwa wamenyanyua mikono juu wakiwa wameiegesha kwenye dirisha wakiwa wameshika bendera nyeusi ikiwa na maandishi ya kiarabu.
Waziri Mkuu wa Australia Tony Abbot amesema tuki hilo linahuzunisha sana.
Abbot amesema haijajulikana nani alihusika na tukio hilo hata hivyo anahisi huenda ni njama za kisiasa na kuwa tayarikamati ya usalama ya taifa imepewa taarifa.
Kamishna wa Polisi wa South Wales Andrew Scipione amesema tukio hilo halichukuliwi kuwa la kigaidi lakini imethibitishwa kuwa kuna mtu mwenye silaha anayewashikilia mateka watu kadhaa.
Mashahidi wa tukio hilo wamesema walimuona mtu akiwa na begi na silaha akiingia kwenye mgahawa, polisi wamefunga eneo hilo, barabara na kuwaondoa watu katika eneo hilo.

No comments: